Na Sultani Kipingo
Kamati ya maandalizi ya Kombe la Dunia 2014 ilikuwa na nyota watano wa zamani wa Brazil (pichani wakiwa na maafisa wa chama cha soka cha Brazil) waliowahi kuwika katika michuano hiyo tokea mwaka 1958 ilipofanyika nchini Sweden. Kamati hiyo, iliyoundwa January 2013 inaundwa na wachezaji wakongwe kina kutoka kushoto juu:
Amarildo Tavares da Silva (wa tatu toka kulia) , José Roberto Gama de Oliveira (Bebeto), Carlos Alberto Torres, Marta Vieira da Silva, Ronaldo Luis Nazario de Lima (wa pili kulia) na  Mário Jorge Lobo Zagallo (kushoto).
Watano kati ya wanakamati hao ambao wamepewa Ubalozi wa FIFA waliwahi kuchezea Brazil wakati nchi hiyo ilipofanikiwa kunyakuwa kombe hilo la dunia. Nao ni Mário Zagallo (mwaka  1958 nchini  Sweden), Amarildo (waka 1962 nchini Chile), Carlos Alberto (mwaka  1970  nchini Mexico), Bebeto (waka  1994 nchini Marekani), na Ronaldo (mwaka  2002 nchini Korea ya kusini na Japan).
Balozi mwingine ni mwanamama Marta Vieira da Silva ambaye ni mshindi mara 5 wa tuzo ya Mchezaji Bora wa FIFA kwa wanawake katika miaka ya  2006, 2007, 2008, 2009 and 2010.
Ronaldo alisema baada ya kuteuliwa: “Ni muhimu tukawa makini maana mbele yetu tuna kazi ya kuangalia maendeleo ya ujenzi wa viwanja, kuchagua mahali ambapo timu ya Taifa itapiga kambi na viwanja mahususi vya mazoezi, na pia kufikia maamuzi muhimu ya kihistoria kama vile kuzindua kauli mbiu ya michuano na Mwanasesera wa Kombe la Dunia la FIFA.”


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...