Na Sultani Kipingo
"BRAZUCA" ni neno jipya lililo midomoni pa wengi ulimwenguni hivi sasa, japo si watu wote wanaojua maana yake. Subiri nikupashe.
"Brazuca" si kitu kingine bali ni  jina la mpira  unaotumika katika michuano ya Kombe la Dunia inayoendelea chini Brazil hivi sasa. 

Neno hilo lina maana mbili. Ya kwanza ni neno la nchi hiyo kwa wa-Brazil wanaoishi nje ya nchi – yaani Diaspora. Maana ingine, neno hilo lina maana ya kujivunia, kuufurahia na kutambia u-Brazil kwa watu wa nchi hiyo, ama kitu ama jambo lolote la kusisimua linalohusiana na nchi hiyo.

Baadhi ya mipira ya Kombe la Dunia imekuwa maarufu kuliko mingine, huku wachezaji wakiilalamikia kwa kile wanachosema mipira hiyo  husafiri kwa kasi zaidi hewani, kiasi hata kusumbua walinda milango
Adidas, watengenezaji maalumu wa mipira kwa ajili ya Kombe la Dunia tokea mwaka 1970, waliuita “Jabulani” mpira uliotumika katika fainali hizo mwaka 2010 huko Afrika Kusini, na kulakiwa na kila aina ya makelele kuwa mwendo wake hautabiriki.
Huu wa sasa jina lake rasmi ni "Adidas Brazuca" na umetengenezwa na kampuni ya Forward Sports  ya Sialkot nchini Pakistan. Jina “Brazuca” la mpira huo lilizinduliwa September 2, 2012 jijini Rio de Janeiro, kupitia kura ya maoni iliyoendeshwa na Fifa na Adidas, ambapo wapiga kura zaidi ya milioni moja wa Brazil walilichagua kwa kura 77.8% dhidi ya majina mengine mawili yaliyopendelkezwa – “Bossa Nova (14.6%) na Carnavelesca (7.6%)


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...