Wananchi wa Kijiji cha Kitwai A wakiwa wamenyoosha mikono juu,kwenye mkutano wa hadhara,wakati Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana alipokuwa akimuunga mkono jambo Mbunge wa jimbo la Simanjiro,Mh Christopher Ole Sendeka,katika suala zima la Utekelezaji wa Ilani ya CCM.
Pichani mbele ye bango kulia ni jengo la Mama na Mtoto la kituo cha Afya Orkesument,Wilayani Simanjiro,ambalo pia Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana alikagua na kujionea ujenzi wake.
Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana akimsikiliza Dkt.Juma Nahonyo wakati wa ukaguzi wa jengo litakalokuwa bohari ya Dawa katika kituo cha Afya cha Orkesument,kulia ni Mbunge wa jimbo la Simanjiro,Mh Christopher Ole Sendeka.

Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Abdulrahman Kinana akizindua gari la mradi wa Kukodisha la Kikunndi cha Vicoba Mkombozi chenye wanachama wapatao 30,mjini Orkesument,Wilayani Simanjiro mkoani Manayara.
Kinana ameambatana na Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye,wako moani Manyara kwa ziara ya siku saba ya Kukagua kuhimiza na kusukuma miradi ya maendeleo inayotekelezwa kwa kufuata Ilani ya Chama,kukagua maandalizi ya uchaguzi ya serikali za mitaa,kusikiliza kero za wananchi na kuzitafututia ufumbuzi.
Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Abdulrahman Kinana akizindua mradi wa Kikundi cha Mazingira kilichopo mjini Orkesument,Wilayani Simanjiro mkoani Manayara.Kikundi hicho kitatumika kuwaelimisha wananchi wa mji huo katika masuala ya usafi na kulinda mazingira,kuwaelimisha wananchi kuhusiana na mambo ya maambukizi ya UKIMWI,masuala ya Rushwa na mengineyo.

Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akipata maelezo mafupi kutoka kwa Mbunge wa Jimbo la Simanjiro,Mh.Ole Sendeka wakati akiangalia josho la ng'ombe la Orkirung'rung ambapo  kuna mradi wa ufugaji wa ng'ombe chotara,ufugaji wenye tija na unaosaidia kuongeza thamani mifugo.
Baadhi ya Wanahabari pichani kati shoto ni Mwinshehe kutoka gazeti la Jambo Leo na Mary kutoka Gazeti la Nipashe wakiwa sambamba na wafuasi wa chama cha CCM,wakifuatilia yaliyokuwa yakijiri kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika katika kijiji cha Kitwai A,wilayani Simanjiro mkoani Manyara kwenye zaiara ya Katibu Mkuu wa CCM.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...