Waziri Mkuu Mhe.Mizengo Pinda akizungumza na warembo kutoka Vyuo vya Elimu ya Juu watakao shindana usiku wa leo Mei 7, 2014 kumpata Mrembo wa Vyuo Vikuu hapa Nchini.Shindano hili litafanyika katika Hoteli ya Royal Village Mjini Dodoma.Warembo kumi na sita watapanda jukwani kumtafuta mshindi.
Nahodha wa Timu ya Bunge, Mhe. Iddi Azzan (wa pili kulia) akipokea Jezi zitakazo tumiwa na Timu ya Soka Bunge kutoka kwa Meneja Mkuu Uendeshaji wa Bank ya ACB, Bi. Juliana Swai,wengine pichani (kushoto) ni Meneja wa ACB tawi la Dodoma Bw.John Magigita,Mkuu wa kitengo cha Masoko na Mawasiliano Bw.Fredrick Archard(kulia),Damas Yusto Msimamizi Idara ya Utawala ACB(wane kulia) na (watatu kulia) ni katibu wa timu ya soka Bunge Bw.Waziri Kizingiti.
Nahodha wa Timu ya Bunge,Mhe.Iddi Azzan wa pili kulia akizungumza na kikosi chaTimu ya Akiba Commercial Bank -ACB kitakacho pambana na timu ya soka ya Bunge kesho.Wa kwanza kulia ni katibu wa timu ya soka Bunge Bw.Waziri Kizingiti.
Naibu Waziri wa Fedha Mhe Mwigulu Nchemba akiwa na Kikosi cha Timu ya Soka cha Akiba Commercial Bank na wafanyakazi kitakacho pambana na timu ya soka ya Bunge katika Uwanja wa Jamhuri Mjini Dodoma leo Mei 7, 2014 mbele ya jengo la ukumbi wa Bunge.Mpambano huo utaanza saa kumi jioni.
Naibu Waziri wa Fedha (mwenye skafu) akiwa na baadhi ya wachezaji na wafanyakazi wa Akiba Commercial Bank. Picha na Na Deusdedit Moshi Mtendaji Mkuu wa Photo Solutions wawakilishi wa Michuzi Blog Kanda ya Kati.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...