Waziri wa nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano) Mhe. Samia Suluhu Hassan akizungumza wakati wa ziara yake katika makao makuu ya DW Swahili Radio mjini Bonn
Mkurugenzi msaidizi idara ya Mazingira katika Ofisi ya Mkamu wa Rais Bw. Richard Muyungi katika Mahojiano na Mtangazaji wa DW Radio Bw. Sudi Mnete kuhusu kilimo rafiki na mazingira na mkutano wa makataba wa mabadiliko ya tabia nchi unaoendelea mjini Bonn.
Mh. Samia Suluhu Hassan aliyekaa, akiwa na mtangazaji wa Radio DW idhaa ya kiswahili Bw. Sudi Mnette akiandaa mitambo kabla ya mahujiano ya masuala ya Muungano, mchakato wa katiba mpya na mkutano wa makataba wa mabadiliko ya Tabia nchi unaoendelea mjin Bonn Ujerumani.
Mhe. Samia Suluhu Hassan (kulia) Mkurugenzi Msaidizi ofisi ya Makamu wa Rais mazingira Bw. Richard Muyungi (wa pili kushoto) Mkuu wa Idhaa ya Kiswahili wa DW Bi. Andrea Shmidt (kati) Mkuu Msaidizi wa Idhaa hiyo Bw. Mohamed Abdul-Rahman (kushoto) na Mtangazaji mkongwe Bi.Uoumirkheir Hamidu (wa pili kulia) na watumishi wa Idhaa ya kiswahi ya radio DW wakati wa ziara katika kituo hicho iliyoambatana na mahojiano ya masuala ya mkutano wa mkataba wa mabadiliko ya tabia nchi unaoendelea mjini Bonn. Picha zote na Evelyn Mkokoi
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...