MSHINDI wa Chemsha Bongo ya Brazil inayoendeshwa na gazeti la Championi, Afande Jamila Omari Mkele, leo amekabidhiwa king'amuzi na dishi kutoka Azam TV pamoja na televisheni ya kisasa (flat screen) kutoka kampuni ya Sony baada ya kushinda shindano hilo.

Makabidhiano hayo yamefanyika leo katika ofisi za Global Publishers wachapishaji wa magazeti ya Uwazi, Amani, Risasi,  Ijumaa,  Championi na Ijumaa Wikienda.
Afisa Masoko wa Azam TV, Shah Mrisho (kulia) akimkabidhi zawadi zake Afande Jamila.
Afande Jamila baada ya kukabidhiwa zawadi zake.
Afisa Masoko wa Global Publishers, wachezashaji wa Bahati Nasibu hiyo, Innocent Mafuru, akiongea na wanahabari baada ya mshindi kukabidhiwa chake.
Afisa Masoko wa Azam TV, Shah Mrisho, akiwaeleza jambo wanahabari (hawapo pichani).
PICHA : RICHARD BUKOS / GPL     

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...