Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (Nida), Dickson Maimu akimkaribisha Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mwamini Malemi (wapili kulia) katika Banda la Nida kujifunza masuala mbalimbali ya kiutendaji yanayofanywa na Mamlaka hiyo iliyopo Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi katika Maonyesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayoendelea jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Afisa Habari wa Wizara hiyo, Christina Mwangosi.
 Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mwamini Malemi (kulia) akimsikiliza kwa makini Afisa Tawala Mwandamizi wa Idara ya Wakimbizi, Jenita Ndone wakati alipokuwa anaeleza majukumu ya Idara hiyo ambayo inasimamia masuala ya wakimbizi nchini, wakati wa Maonyesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayoendelea katika Viwanja vya Manzi Mmoja, jijini Dar es Salaam.
 
 Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mwamini Malemi (kushoto) akimuuliza maswali Afisa wa Idara ya Uhamiaji, Mathew Ikomba kuhusu matatizo mbalimbali likiwemo baadhi ya wananchi wanailalamikia Idara hiyo kuhusu uombwaji wa rushwa wakati wanapoomba kupatiwa Hati ya Kusafiria (pasipoti). Malemi aliitaka idara hiyo ifuate haki wakati wananchi wanapoomba pasipoti. Wizara na Idara zake inashiriki katika Maonyesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayoendelea katika Viwanja vya Mnazi Mmoja, jijini Dar es Salaam
 Koplo wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Loyce Abeid, akimuonyesha Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mwamini Malemi (kushoto) kifaa kinachotumika kwa ajili ya uokozi wa magari yanapopata ajali hasa magari ya tenki. Malemi alitetembelea Banda la Wizara na Taasisi zake katika Maonyesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayoendelea katika Viwanja vya Mnazi Mmoja, jijini Dar es Salaam.
 
 Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mwamini Malemi (wapili kushoto aliyekaa kwenye kiti) akiwa katika picha ya pamoja na wafanyakazi wa Wizara yake ambao wapo katika Maonyesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayoendelea katika Viwanja vya Mnazi Mmoja, jijini Dar es Salaam. Kushoto aliyekaa kwenye kiti ni Mkurugenzi wa Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (Nida), Dickson Maimu. Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi. 




Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...