Mtendaji Mkuu wa Barclays PLC, Anthony Jenkins akizungumza na baadhi ya wafanyakazi wa Benki ya NBC Tanzania wakati wa ziara yake nchini jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki. Kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa NBC Tanzania, Bi. Mizinga Melu.
 Mtendaji Mkuu wa Barclays PLC, Anthony Jenkins (kulia) akipozi kwa picha na Rachel Mwalukasa mmoja wa wafanyakazi aliyemkabidhi tuzo kwa kuwa mfano wa kuigwa katika suala la kujitolea binafsi katika kuisaidia jamii. Kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji nwa NBC Tanzania, Mizinga Melu.
 Wafanyakazi wa NBC Tanzania wakionyesha sura ya matumaini wakati wakimsikiliza bosi wao, Antony Jenkins alipokuwa akizungumza kuhusu mikakati ya kimaendeleo ndani ya benki hiyo nchini.
 Baadhi ya wafanyakazi wa Benki ya NBC wakishangilia hotuba ya Mtendaji Mkuu wa Barclays PLC, Anthony Jenkins wakati wa ziara yake nchini Tanzania.
 Mtendaji Mkuu wa Barclays PLC, Anthony Jenkins (kulia) akibadilishana mawazo na Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Bytrade Tanzania Managing Director, Harish Dhutia katika hafla iliyoandaliwa na NBC kwa ajili ya wateja wa makampuni  wakati wa ziara yake nchini Tanzania mwishoni mwa wiki. Kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa NBC Tanzania, Mizinga Melu.
Wafanyakazi wa NBC Tanzania wafuatilia kwa makini hotuba ya Mtendaji Mkuju wa Barclays PLC, Anthony Jenkins wakati wa ziara yake nchini   ambapo alifanya mikutano na wafanyakazi, wateja wa NBC na wadau wengine wa benki hiyo. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. AnonymousJune 02, 2014

    Ninampongeza sana dada Rahel (Recho) Mwalukasa kwa kuendeleza ufanyakazi uliotukuka. Huyu dada akiwa Barclays proper kabla haijanunua NBC alikuwa anapata zawadi za ufanyakazi bora na kupewa hadi treat Dubai. Leo hii alihamia NBC ambayo later Barclays waliinunua na ameendelea kuwa role model. Kwa hakika CRDB walimkosa na sielewi ni kwa nini MD. Kimei alishindwa kum-maintain. Keep it up dada Rahel.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...