Na Allan Ntana, Tabora
SHEKHE wa mkoa wa Tabora Salum Shaban Salum na waumini wenzake watano wamefikishwa kizimbani katika mahakama ya hakimu mkazi mkoani hapa
akikabiliwa na shitaka la kufanya fujo katika msikiti wa Ijumaa mkoani
hapa.
Wakili wa serikali Juliana Changalawe akisoma mashitaka hayo mbele ya
hakimu mfawidhi wa mkoa wa Tabora Issa Magoli alidai kuwa watuhumiwa
hao kwa pamoja
walitenda kosa hilo mnamo tarehe 14 Juni 2014 katika msikiti mkuu wa
Ijumaa uliopo eneo la Gongoni mjini hapa.
Wakili huyo aliiambia mahakama kuwa siku hiyo majira ya mchana
watuhumiwa Shaban Salum, Mgude Ahmed, Said Maganga, Kassim Shomary,
Abubbakar Ludenga na Kassim Rajab walimtoa katika ibada Shekhe
Ibrahim Mavumbi.
Watuhumiwa ambao wanawakilishwa na wakili Mussa Kwikima wa mjini
hapa mara baada ya kusomewa shitaka hilo wote walikana na kesi hiyo
imeahirishwa hadi tarehe 30/06/2014 kwa ajili ya kuanza kusikilizwa kwani
upelelezi umeisha kamilika na wote walipata dhamana.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...