Ubalozi Mdogo wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania uliopo Dubai, UAE, unapenda kuwatangazia Umma wa Watanzania kuwa Kampuni na Wakala wa Ajira ya CAREER FARAH LEISURES ya UAE, imetangaza kazi zifuatazo kwa watu wenye sifa zinazohitajika kuziomba.
Hivyo basi, Ubalozi Mdogo unawaomba Watanzania wenye sifa za kazi zilizotangazwa, kuziomba mara moja na kuwasilisha maombi hayo kama ilivyoonyeshwa kwenye tangazo hapo juu. Aidha, ili kurahisisha ufuatiliaji wa maombi yenu, tunakuombeni mtume pia nakala ya maombi yenu kwa anuani ya barua pepe ya Ubalozi Mdogo kama ifuatavyo:
tzconsdb@emirates.net.ae.
Attention: Mheshimiwa Balozi Mdogo,
Ubalozi Mdogo wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Dubai, UAE.
Ubalozi Mdogo unapenda kuwafahamisha kuwa, tangazo hili litatolewa pia kwenye Gazeti la Serikali la DAILY NEWS.
Akhsanteni, na tunawatakia kila la kheri waombaji wote.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...