Na Sultani Kipingo 
wa Globu ya Jamii

Uwezo wa kifedha wa Nike unaipaisha kampuni hiyo katika vita vya Kombe la Dunia 2014 kwa kuiongoza kampuni ya Adidas kwa mabao 4 katika awamu ya makundi ya michuano hiyo huko Brazil. 
Kampuni ya Nike ambayo ndio kubwa zaidi duniani kwa vifaa vya michezo imeonesha umwamba wake baada ya nyota inayowadhamini kufunga mabao 61 katika awamu hiyo ya makundi, huku Adidas ikifuatia kwa magoli 57.
 Lakini Adidas wanaweza kupata ahueni kwa kuwa na njumu bora, kwa mujibu wa wataalamu wa mambo hayo. Kiatu cha Adizero kinachovaliwa na nyota wakali kama  Lionel Messi, Robin van Persie, Arjen Robben, Karim Benzema na  Thomas Muller kimechangua magoli 38 katika awamu hiyo, huku kiatu cha Nike cha Superfly IV kinachovaliwa na
Alexis Sanchez  wa Chile na Xherdan Shaqiri wa Uswisi kimepiga mabao 21 hadi sasa (kabla mechi za mtoano kuanza). 
Adidas pia wanaongoza katika chati ya magoli ya kusaidia, kwa kuchangia mabao 65 katika awamu ya makundi, dhidi ya 54 ya Adidas, wakati kampuni ya Umbro ikijikongoja kupata goli, na hadi sasa ina goli moja la usaidizi kwa mchezaji Mauricio Pinilla aliyetoa pasi katika mchezo wa Chile dhidi ya Australia, ila kiatu chao hakijafunga bao hadi sasa. 
Wachezaji wanaovaa kiatu cha Puma wamefunga mabao manane, wakati kampuni ya Mizuno na Warrior kila mmoja akichangia mabao matatu. Kampuni ya Under Armour pia imemaliza awamu ya makundi bila kupata bao. 
 Nike wanaomdhamini Neymar wa Brazil wana mabao 61
  Cristiano Ronaldo wa Ureno anadhaminiwa na  Nike
  Robin van Persie wa Uholanzi anavaa kiatu cha  Adidas aina ya Adizero 
Adidas wanaomdhamini Lionel Mesii wa Argentina wana mabao 57

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...