Eliamini Amon Urio, (Katikati), mzazi wa Eileen, ambaye ni mwanafunzi wa kidato cha tatu shule ya sekondari ya wasichana, Marian, iliyoko Bagamoyo mkoani Pwani, akielezea jinsi fao la elimu litolewalo na Mfuko wa Pensheni wa PPF, linavyosadia kumsomesha motto wake, baada ya kumpoteza mumewe mwaka 2005. Aliyasma hayo wakati wa sherehe za siku ya wazazi ya shule hiyo, Jumamosi Juni 7, 2014. Kushoto ni Meneja Uhusiano na Masoko wa PPF, Lulu Mengele na kulia ni Afisa Michango wa PPF, Kanda ya Kinondoni, Kwame Temu.
Joyce Nachenga, (Kusho), mwakilishi wa Mfuko wa PPF, Kanda ya Kinondoni jijini Dar es Salaam, akiwaeleza wazazi wa wanafunzi wa shule ya sekondari Marian, faida za kujiunga na Mfuko huo, wakati wa sherehe za siku ya wazazi iliyofanyika shuleni hapo Jumamosi Juni 7, 2014.
Mmoja wa wanafunzi wanaofaidika na fao la Elimu, litolewalo na Mfuko wa Pensheni wa PPF, Rosalia Faustin Madulu, (Kulia), akieleza jinsi yeye binafsi ambaye kwa sasa yuko kidato cha Kwanza shule ya sekondari Marian iliyoko Bagamoyo, jinsi anavyofaidika na fao hilo tangu apoteze mzazi wake miaka 9 iliyopita. Aliyasema hayo wakati wa siku ya wazazi ya sekondari hiyo, Jumamosi Juni 7, 2014.Wakwanza kushoto ni Meneja Uhusian na Masoko wa PPF, Lulu Mengele, na wengine ni wanafunzi wengine wa shule hiyo wanaofaidika la fao hilo, Deborah Kibona, (Wapili kushoto) na Eileen Amon Urio.
Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu la Dar es Salaam, Kanisa Katoliki, Muadhama Policarp Kadinali Pengo,akinzungumza wakati wa sherehe za siku ya wazazi ya shule ya sekondari ya wasichana, Marian, iliyoko Bagamoyo mkoani Pwani, Jumamosi Juni 7, 2014.
Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu la Dar es Salaam, Kanisa Katoliki, Muadhama Policarp Kadinali Pengo, akimshukuru Meneja Uhusiano na Masoko wa Mfuko wa Pensheni wa PPF, Lulu Mengele, kutokana na Mfuko huo kudhamini sherehe za siku ya Wazazi ya sekondari za Marian, huko Bagamoto, mkoani Pwani Jumamosi Juni 7, 2014.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...