Na Greyson  Mwase, Tarime

Naibu Waziri wa Nishati na Madini anayeshughulikia madini Stephen Masele amekemea vikali tabia ya wamiliki wa migodi  kuajiri watoto wenye umri wa chini ya miaka 18  kwani inarudisha maendeleo ya watoto hao na kwa jamii kwa ujumla inayowategemea

Waziri Masele ameyasema hayo kwenye ufunguzi wa semina iliyoshirikisha wachimbaji wadogo, madiwani, viongozi wa vijiji, wilaya, madiwani pamoja na viongozi wa vyama  vya siasa inayoendelea katika jimbo la Mwibara wilaya ya Bunda mkoani Mara.

Waziri Masele alisema kuwa kumekuwepo na tabia ya wamiliki wa migodi, ikiwa ni pamoja na wazazi wenye watoto wenye umri chini ya miaka 18 kuruhusu watoto hao kufanya kazi kwenye migodi badala ya kuwahimiza kwenda shule na kupata elimu itakayowasaidia kutoka kwenye giza.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 2 mpaka sasa

  1. AnonymousJune 07, 2014

    wazazi wawajibike watoto waende shule siyo kutafuta pesa za kujikimu wakiwa wadogo.

    ReplyDelete
  2. AnonymousJune 08, 2014

    Inapiga marufuku lakini utekelezaji utakuwaje?

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...