Kwanza nianze kwa kuwatakia Waislamu wenzangu wote Mfungo mwema wa mwezi wa Ramadhani na Kheri za mfungo huu zimulike katika nyumba zote, nchi zote na wale wote ambao kwa namna moja au nyengine wameshindwa kufunga mwezi huu kwa sababu mbalimbali ikiwemo hali duni ya maisha, maradhi au kubanwa na hali ambazo zinawalazimu wasipate thawabu za funga.Ni imani Mungu mwenyezi atawaangazia na kufanya wepesi kuwaondoa katika hali hiyo.

Niwaombee salaam Wadogo zangu waliotekwa Nigeria, na wale wanaoishi katika mazingira hatarishi kama vita.Kwangu ni dua kipindi hiki ili kuweka wepesi katika kuwatoa katika dhiki hizo kubwa.

Pia nitumie nafasi hii kuuambia Umma wa Tanzania na hasa wale watumiaji wa mitandao ya kijamii ambao wameendelea kuwa waathirika wa matumizi mabaya ya mitandao kuwa Hii ndiyo Account rasmi ya Ridhiwani Kikwete.Hizo account zingine ikiwemo

Ridhiwani J. Kikwete
Ridhiwani Kikwete official fan page
Ridhiwani Kikwete birth date 1983
Ridhiwani Jakaya Kikwete
Ridhiwani Kikwete -nimevaa shati la Ccm

Na nyenginezo si account zangu,ni za watu ambao wamejisikia kutumia jina langu kwa sababu mbalimbali jambo ambalo nimeona katika siku hii ya leo nilikanushe. Kwa kauli ya kukanisha namaanisha kuwa hizi account sina mahusiano nazo kabisa na hawa wanaotumia Jina langu nawaomba waache mara moja kwani si jambo jema kuoongopea ummma wa Watanzania ambao wamekaa mitandaoni wakiamini wanafanya mawasiliano nami wakati kihalisia si mimi.

Mwisho, napenda kuwaambia Watanzania na wana mtandao wenangu kuwa haya Makundi yaliyoanzishwa kwenye mtandao kama

-YOUTH BATTLE
-VIJANA WANAOIPENDA NCHI YAO KWA MOYO
-SACCOS INAYOTOA MIKOPO
-UNGANISHAJI BODI YA MIKOPO etc.

Na mengineyo ni makundi ambayo  sijawahi na wala sijashiriki kuyaasisi mimi.Ni hao ambao hawana nia njema na jina langu na heshima ya familia  ambayo nimekuwa nahangaika kuihifadhi.

Account yangu halisi ni

RIDHIWANI KIKWETE ambayo kwenye profile picha yangu yuko bwana Reginald Mengi na Juzi nilitoa tangazo kukanusha habari za msiba wa Ndg.Shukuru Jumanne Kawambwa(Mb) wa Bagamoyo.

Hivyo naomba kutoa angalia kwa Watanzania wenzangu.

Nawaomba kuwasilisha.
Mimi

RIDHIWANI KIKWETE.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 2 mpaka sasa

  1. AnonymousJune 30, 2014

    Naomba nikutie moyo ndugu yangu yote unayopitia ikiwemo kupewa kila kitu cha ufahali kwamba ni mali zako na mashambulizi mengine, hayo yote yanakuandaa na kukukomaza kuwa mwanasiasa na Kiongozi shupavu. Keep it up and don lose heart. Its me Bishop

    ReplyDelete
  2. AnonymousJune 30, 2014

    NINGEOMBA VITAMBULISHO VYA URAIYA VILIPIWE ANGALAU GHARAMA KIDOGO KANI WATANZANIA HAWAJAJUWA UMUHIMU WA ID. WENGI WETU WANAVIACHA KWENYE MADUKA YA PHOTO COPY KWA GHARAMA YA Tsh 200/= HASWA WANAPO KOSA CHENJI YA KULIPIA COPY ZAO WANAVIWEKA REHANI NA HAWARUDI KUVIKOMBOWA NIMEKUTA VITAMBULISHA VYA WAPIGA KURA ZAIDI YA SABA VIMEBANDIKWA KWENYE DIRISHA LA DUKA MOJAWAPO MJINI BIHARAMULO OFISI YA COPY KWA MR KHATRY NA KWENGINEKO MWANZA BUKOBA KAHAMA. KAMA HAMNIAMINI PITIENI KWENYE MADUKA YA PHOTO COPY NCHI NZIMA UTAKUTA HALI NDIO HIYOOOO

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...