Waziri wa Nishati  na Madini Profesa Sospeter Muhongo akiongea wakati wa mkutano wa Mawaziri wanaohusika na  masuala ya   Nishati ambapo aliwatangazia wajumbe hao kwamba Tanzania itakuwa mwenyeji wa Mkutano wa  Bara la Afrika  kuhusu  Nishati Endelevu katika muda utaopangwa na Umoja wa Mataifa.
 Ujumbe wa Tanzania katika Mkutano wa siku tatu wa Nishati Endelevu kwa Wote ( SE4ALL)  ulioandaliwa na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa.  Eng. Yahya  Samamba Katibu wa Waziri na  Eng. Styden Rwebangila
Watanzania wengine ambao ni sehumu ya Ujumbe wa Tanzania.  Kutoka  kushoto ni  Bi. Venosa Ngow ( TPDC) Eng. Leonard Masanja kutoka Wizara ya  Nishati na Madini na  Eng Jones fredrick Olutu kutoka  Wakala wa Nishati  Vijijini ( REA)
---------------------------------
Na  Mwandishi Maalum,  New  York
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  imeelezea utayari wake wa  kuwa mwenyeji wa mkutano wa Bara la Afrika kuhushu Nishati Endelevu kwa wote.
Ahadi hiyo imetolewa  siku ya Ijumaa,  na Waziri wa Nishati na Madini ,  Profesa Sospeter Muhongo ( Mb) mwishoni wa mkutano  wa siku tatu , uliojadili kwa kina upatikanaji wa nishati endelevu kwa wote. Mkutano huu  uliojumuisha wadau wa kada mbalimbali uliandaliwa na  katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa,  ambapo pia  palifanyika    uzinduzi wa mwongo wa nishati endelevu kwa wote unaoanza 2014 hadi 2024.
“  Ninapenda kutaarifu kwamba,  nimezungumza na   Rais wangu, Tanzania iko tayari kuwa mwenyejiji  wa mkutano wa nchi za Afrika kuhusu nishati endelevu. Tutakuwa  wenyeji wa mkutano huo pale Umoja wa Mataifa utakapokuwa tayari”. akasema  Waziri Muhongo. Kauli iliyopokelewa vema na waandaji wa mkutano huo.
Waziri Muhongo ambaye ameshiriki  kikamilifu mijadala mbalimbali tangu mwanzo wa mkutano hadi mwisho, alisema Tanzania na kama  ilivyo kwa nchi nyingine nyingi hasa za Afrika,  Nishati Endelevu ni muhimu  katika utekelezaji na ufanikishaji wa  Maendeleo  Endelevu  badaa ya  mwaka 2015.
Akasisitiza kuwa katika utekelezaji wa mpango wa  nishati mbadala kwa wote,  Afrika  inapashwa kupewa kipaumbele cha pekee.
Katika siku hii ya tatu na ya mwisho ya mkutano huu,  Mawaziri walioziwakilisha nchi zao, walipata fursa ya kubadilishana mawazo,  kuelezea uzoefu wao,  kutoa maoni yao na  halikadhalika kupendekeza nini  cha kufanya ili hatimaye watu wengi zaidi hususani katika nchi zinazoendelea  waweze kupata huduma hii ya nishati endelevu.
Inakadiriwa kwamba  zaidi ya  watu 1.3 bilioni duniani kote hawana huduma ya umeme na zaidi wa 2.6 bilioni wanatumia nishati asilia kwa  kupikia na  kupata joto. Matumizi ya  nishati asilia yanasababisha    watu  4.3 milioni kufariki kila mwaka  kabla ya wakati  wao  huku wengi  kati yao wakiwa ni   wanawake na watoto  kutokana na uvutaji wa  moshi.
Waziri Muhongo ambaye ameongoza  ujumbe wa  Tanzania katika mkutano huu  akiwamo  Muhandisi kutoka  Wakala wa Nishati  Vijijini. Amesisitiza pia  uhusiamo kati ya   nishati na elimu   kwa kile alichosema ili mwanafunzi aweze kujiandaa au kujisomea vizuri anahitaji nishati ambayo ni endelevu na yenye  uhakikia.
 “ Hii itakuwa mara yangu ya nne  kutoa maoni na mchango wangu na  kwa sababu hiyo  nisingepeda kutumia muda  mwingi na  pengine kurudia  kile ambacho nimeshakisema huko nyuma. Nisisitize kwamba tunapozungumzia mpango wa  nishati endelevu kwa wote basin chi za afrika  zinatakuwa kupewa kipaumbele cha pekee,  vile vile  suala  la uwepo wa nishati endelevu lina uhusiano mkubwa na utekelezaji wa maendeleo endelevu baada ya  2015.
Akasisitiza kuwa Tanzania  imejipanga vema katika kuhakikisha kwamba  wananchi wake wanapatiwa huduma  hiyo muhimu kwa maendeleo yao na  nchi kwa ujumla.
Akinukuu wanafalsafa mbalimbali,  Waziri Muhongo amebainisha kwamba  dhana hiyo ya kumpatia  huduma ya nishati endelevu  kila mtu inawezekana   ikiwa kila mmoja atatimiza wajibu wake pamoja na ushirikiano.
Baadhi ya wazungumzaji katika mkutano huo wa  Mawaziri walieleza kwamba  inawezekana kabisa kutumia mifano  ya huduma za  usambazaji  wa simu za mkononi huduma ambayo imewafikia watu wengi ikatumika katika usambazaji wa  nishati  endelevu.
Wengine walisisitiza umuhimu wa nishati mbadala kama vile wa matumizi ya nguvu za jua na upepo kama moja wa  eneo muhimu la kuwafikia watu wengi. Huku baadhi wakisisitiza  umuhimu wakuwatumia wataalamu waliopo pamoja na tafiti ambazo zimekwisha kufanyika kuhusu suala zima la nishati. 





Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...