Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Dkt. Mahadhi Juma Maalim (Mb.) kwa pamoja na Katibu Mkuu wa Wizara ya Kazi na Ajira wa Qatar wakisaini Mkataba wa Kazi ambao unalenga kuwawezesha Watanzania hususan vijana wenye ujuzi/taaluma katika fani mbalimbali kupata fursa za ajira na kazi za staha, ujira stahiki, kujiunga na hifadhi za jamii nchini Qatar.  Mkataba huo pia unazingatia sheria na viwango vya kazi kulingana na Mikataba ya Kimaataifa ikiwemo ya Shirika la Kazi Duniani (ILO).
Mhe. Dkt. Maalim akiwa katika mazungumzo na Katibu Mkuu wa Wizara ya Kazi na Ajira wa Qatar mara baada ya kusaini Mkataba wa Kazi kati ya nchi hizo mbili. Kulia ni Balozi Simba Yahya, Mkurugenzi wa Idara ya Mashariki ya Kati katika Wizara ya Mambo  ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa.

Mazungumzo yakiendelea.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...