Pichani ni  Meneja wa Tawi lililopo ndani ya  maonyesho ya biashara ya Kimataifa ya 38 yanayoendelea kwenye viwanja vya Mwal.Julius Nyerere jijini Dar,Bi. Upendo Tendewa akifafanua zaidi huduma zitolewazo na benki hiyo.Bi.Upendo amesema kuwa dhamira yao kubwa ni kukidhi mahitaji ya wateja ya kibenki na ya kifedha kwa kuhakikisha upatikanaji wa bidha na huduma bora kabisa katika soko  kwa bei inayowezekana kulipa na viwango  vyenye manufaa yanayolingana na gharama na faida ya kurudhisha kwa mwanahisa.

Amesma benki hiyo inatumia kadi yako iitwayo Twiga ExpressCard ambayo mteja anaweza kuitumia kupata huduma za kibenki katika ATM yoyote iliyounganishwa na mtandano wa UMOJA SWITCH,ambapo zaidi ya ATM 180 na mabenki ishirini nna nne nchini yameunganishwa.
 Afisa Masoko wa Benki ya Twiga Bancorp Bwa.Adalbert Alchard akizungumza na Wanahabari nje ya banda lao kuhusiana na huduma mbalimbali zitolewazo na benki hiyo kwa wateja wao, kwenye maonyesho ya biashara ya Kimataifa ya 38 yanayoendelea kwenye viwanja vya Mwal.Julius Nyerere jijini Dar.Pichani kushoto ni  Afisa wa Benki hiyo,Bi Tuddy Lutengano. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...