Na  Francis Godwin Blog.


DIWANI  wa  chama   cha Tanzania Labour Party (TLP) kata ya  Lupingu  wilaya ya  Ludewa mkoani  Njombe  John Kiowi amempongeza  mbunge wa  jimbo la Ludewa  Deo Filikunjombe kwa jitihada zake   anazozifanya katika  kuwapelekea maendeleo wananchi wa Ludewa  huku akiwashangaa   wapinzani wanaopinga  jitihada  mbali mbali  zinazofanywa na serikali ya  chama  cha Mapinduzi (CCM) na  kudai  kuwa  yeye  si mpinzani wa uchwara wa  kupinga  maendeleo .

Akizungumza   na  wanahabari  jana wakati wa  zoezi la mbunge  Filikunjombe  na  diwani  huyo  kushiriki na  wananchi  wa kata ya  Lupingu  kuchimba mashimo ya nguzo  za umeme  na kusimika  nguzo hizo za umeme , Kiowi  alisema  kuwa   ni  zaidi ya  wabunge  watano  wamepata  kuliongoza  jimbo  hilo la Ludewa  ila ni mara  yake ya kwanza  kuona mbunge akishiriki bega kwa  bega na wananchi wake  kuchimba mashimo  kama ambavyo mbunge  huyo anafanya .

" Jamani  wananchi  kwanza ni jambo la kumpongeza mbunge  wetu mbali ya kuhimiza wananchi ila mwenyewe  pia amekuwa mstali wa mbele katika  kushiriki tofauti na wana siasa  wengine ambao  muda  wote  wao ni watu wa majukwaani ila  vitendo sifuri .....nasema  Ludewa  imempata mbunge na niweke  wazi  hapa mimi  sio mpinzani hivi  tujiulize wenyewe  nikisema mimi ni mpinzani napinga  nini hapa haya maendeleo  ni kwa  faida yangu na  wananchi  wote  sasa kama mbunge wa CCM wanafanya  kuna haja ya upinzani hapa ".

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...