Katika ziara yake Mkoani Mara Dkt.Magufuli alifanya ziara Kijiji cha Mwibara (M/Kiti - TLP), Kata ya Mwibara (Diwani-TLP) Jimbo la Mwibara (Mbunge - CCM). 
Akiwa katika kijiji cha Mwibara alifungua kombe la Kangi Lugola kisha kuhutubia wananchi. Kwa upendo M/Kiti na Diwani wa kata ya Mwibara wote kutoka TLP- walimzawadia Mbuzi wawili. Aidha, Magufuli aliweza kuzoa wanachama wapya zaidi ya 200 kata ya Mwibara na akafanya mkutano kata jirani ya Iramba na kuzoa wanachama wengine zaidi ya 150. 
 Dkt.Magufuli aliweza kuchangia kiasi cha shilingi milioni moja kwenye mfuko wa maendeleo wa jimbo hilo. Jimboni kwa Nimrodi Mkono alizindua kivuko kipya cha MV Mara kitakachofanya safari zake kati ya Jimbo la Mwibara (Iramba) kwenda Jimbo la Musoma Vijijini (Majita). 
Kivuko hiki kimeigharimu serikali shilingi milioni 545.2. Awali wananchi walisafiri kilomita 240 lakini kwa kutumia kivuko hiki watatumia dakiki 30 tu, zaidi ya hapo nauli walikuwa wakilipa shilingi 2000/- kwa mtu mmoja lakini kwa kivuko hiki kipya nauli ni shilingi 500/- na wanafunzi bureee! 
 Dkt.Magufuli pia aliweza kukagua ujenzi wa barabar ya Bunda - Kisorya sehemu ya Kisorya - Bulamba inayojengwa kwa shilingi bilioni 51.1/-. 
 Waliohudhulia: Kangi Lugola (MB), Nimrodi Mkono(MB),Mhandisi Iyombe (Katibu Mkuu Wizara ya Ujenzi), Mhandisi Evarist Ndikilo (RC-Mwanza & Ag.Mara), Ester Bulaya (MB-Viti Maalum), Wenyeviti wote wa Bodi zilizo chini ya Wizara ya Ujenzi, Kamati ya Ulinzi ya Mkoa n.k
 Dkt.Magufuli akifungua michuano ya  kombe la Lugola kwa kupiga penati golikipa akiwa Kangi Lugola, wanaoshuhudia ni Mhandisi Iyombe (Katibu Mkuu Wizara ya Ujenzi),Mhandisi Evarist Ndikilo (RC-Mwanza & Ag.Mara). Matoke, Magufuli alifunga goli.
Golikipa Kangi Lugola baada ya kupangua penati ya Magufuli...Hadi refa alishangilia!
Dkt.Magufuli akizawadiwa Mbuzi wawili 
Wananchi wakinyoosha mikono kuapa kujiunga na Chama cha Mapinduzi (CCM) kata ya Mwibara 
Dkt.Magufuli, Mhe Kangi Lugola na Mhe Nimrodi Mkono wakikata utepe kuashiria uzinduzi wa MV.Mara

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...