Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Ban Ki Moon, akifungua mkutano wa siku moja wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa ambapo siku nzima ya Alhamisi liLIjadili ajenda ya uwekezaji kwa Afrika na mchango wake kwa Maendeleo endelevu. Katika hotuba yake, Ban Ki Moon alisema Afrika isiridhike na ukuaji wa jumla wa uchumi wake ambao umekuwa ni mzuri bali inahitaji kuwekeza zaidi ili uwekezaji huo uweze kuchangia katika kuleta maendeleo endelevu, kuwaondolea watu wake umaskini, kukuza ajira na kipato na kwamba Afrika ilihitaji kuwekeza zaidi katika miundombinu, kilimo na nishati endelevu pamoja na mambo mengine.
Muwakilishi wa Kudumu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Balozi Tuvako Manongi akizungumza wakati wa mkutano kuhusu uwekezaji katika Afrika. Katika mchango wake, alisisitiza kuwa pamoja na Afrika kuchagizwa kuvutia uwekezaji zaidi pamoja na ukusanyaji wa mapato ya ndani Jumuiya ya kimataifa inatakiwa kutoa ushirikiano usio na shaka katika udhibiti wa ukwepaji mkubwa wa kodi, utoroshwaji na biashara harafu ya fedha na ambayo inazinyima nchi za Afrika mapato ambayo yangeweza kutumika katika utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo na hivyo kuwaondoelea wananchi wake umaskini uliokithiri.


.jpg)
.jpg)
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...