Afisa Biashara Mkongo wa Taifa wa mawasiliano,Bwa.Thomas Lemunge akielezea kuhusiana na Mkongo wa Taifa wa mawasiliano unavyofanya kazi, mapema leo ndani ya maonesho ya 38 ya Biashara ya Kimataifa yanayoendelea hivi sasa jijini Dar Es Salaam.

Bwa.Thomas amebainisha kuwa Mkongo wa Taifa wa mawasiliano umekwisha sambaa maeneo mengi ikiwemo mikoa 21 ya Tanzania mpaka sasa,Amesema kuwa Makampuni yote ya ndani yanatumia mkongo huu wa mawasiliano kupeleka huduma kwa wananchi na kuongeza kuwa Mkongo huo unaunganisha mataifa mbalimbali kupitia mkongo huu wa Taifa wa Mawasiliano ambao umerahisisha mambo mengi katika jamii ikiwemo suala zima la mawasialiano ya simu za kiganjani na mambo mengineyo.

Bwa.Thomasa amewataka wananchi kuhakikisha wanautunza na kuulinda Mkongo huo wa mawasiliano ili kuendelea kurahusisha upatikanaji wa huduma mbalimbali.
Afisa Mahusiano wa kampuni ya Simu ya TTCL-Tanzania,Bwa.Edwin Mashashi akielezea  kuhusiana na huduma zao mbalimbali zitolewazo na kampuni hiyo,ikiwemo masuala ya Internet na huduma nyinginezo mbalimbali kwa wateja wao.

Bwa.Edwin ameeleza kuwa kwa sasa kampuni yao iko katika mchakato mkubwa wa kuziboresha huduma zao ziwe na ubora zaidi,ameongeza kusema kuwa pia Wanatarajia kufunga Wi-Fi katika maeneo mbalimbalu ya jiji la Dar, ambapo gharama itakuwa ni ya bei nafuu.

Edwin amesema kuwa Kampuni ya TTCl-Tanzania,wanatarajia kuzindua kituo kikubwa Afrika Mashariki cha kuuzia internet,kituo hicho kinatarajia kuzinduliwa mwishoni mwa mwezi Julai ama Agosti,''mtambo huo tayari umekwishafungwa hapa hapa nchini tayari kwa kuanza kutoa huduma hiyo Afrika Mashariki,hivyo kutakuwa hakuna haja tena ya kununua tena Internet nje'',amedema Bwa.Edwin.
 Pichani ni baadhi ya wateja wakipata maelezo maelezo mbalimbali kuhusiana na huduma zitolewazao na Kampuni ya simu TTCL,ndani ya banda la kampuni hiyo ndani ya maonesho ya 38 ya Biashara ya Kimataifa yanayoendelea hivi sasa jijini Dar Es Salaam.
 Wahudumu wa TTCL wakihudumia wateja wao kwa njia ya simu ndani ya banda lao,katika  maonesho ya 38 ya Biashara ya Kimataifa yanayoendelea hivi sasa jijini Dar Es Salaam.
 Namna mkongo wa Taifa unavyofanya kazi na maeneo mbalimbali ulivyosambaa nchini.
 Baadhi ya Wahudumu wa kampuni ya simu ya TTCL wakiendelea kuwajibika.
Ankal wa tatu kushoto akiwa na Wadau wa TTCL ndani ya banda lao lililopo ndani ya viwanja vya maonesho ya 38 ya Biashara ya Kimataifa yanayoendelea hivi sasa jijini Dar Es Salaam.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. AnonymousJuly 02, 2014

    their customer services is very poor and dont value their customers.Also they internet is not stable it keeps on resetting going down then up itself every now and then.Not stable

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...