Mchezaji wa zamani wa Yanga na Taifa Stars Ally Mayay Tembele (pichani) anawaarifu ndugu, jamaa na marafiki pamoja na jamii ya Tanzania kwa jumla kwamba email address yake ya maya@yahoo.com imeibwa na matapeli na kuanza kutumika vibaya (phishing) kwa kudai kuwa yeye yupo Ukraine na amekumbwa  na matatizo hivyo anaomba msaada wa pesa haraka.

Mbaya zaidi, katika email yake hiyo Ally Mayay Tembele aliwahi kuambatanisha nyaraka nyeti kadhaa ikiwemo pasipoti ambazo wezi hao wanazitumia kama alama ya uthibitisho kuwa wao ni yeye. Hao jamaa ni wezi na waongo wakubwa. Msiwape ushirikiano kabisa.


Ukweli ni kwamba Ally Mayay Tembele yupo Dar es salaam na wala hajasafiri kwenda nje ya nchi hivi karibuni. Hivyo anaomba yeyoye anayeletewa email hiyo ya mayayt@yahoo.com aidharau na wala asitoe ushirikiano wowote na hao watumaji. Ni wezi na matapeli.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...