DSC_0008
Afisa Mradi wa uchumi wa kijani ndani ya hifadhi hai (GEBR) Kitengo cha Sayansi kutoka UNESCO na mwakilishi wa KOICA, Myoung Su Ko, (kulia) akisalimiana na Mtendaji wa Kata ya Mnyuzi, Bw. Gosbert Ishengoma mara baada ya kuwasili kwenye ofisi za kata hiyo wilayani Korogwe. Katikati ni Afisa Usafi na Mazingira wa Wilaya ya Korogwe, Bw. Frederick Linga.

Na Mwandishi wetu, Korogwe
Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) limezindua mradi wa mamilioni katika eneo la hifadhi Usambara Mashariki, kwa mafunzo kwa wakazi waliomo na wanaozunguka hifadhi ya Usambara Mashariki.

Mradi huo ambao umelenga kuwainua wanavijiji kiuchumi huku wakitunza mazingira umepata fedha kutoka Shirika la Ushirikiano wa Maendeleo la Kimataifa la Korea ( KOICA).
Mradi huo unaotekelezwa katika vijiji 19 vinavyozunguka Hifadhi Hai ya usambara mashariki ikiwa ni utekelezaji wa mradi wa uchumi wa kijani ndani ya hifadhi hai(GEBR).

Mradi huo utawawezesha wananchi kwenye vijiji hivyo kutumia raslimali zao kwa namna endelevu. Mradi huo unaojulikana kama “Green Economy in Biosphere Reserves (GEBR)”,wenye thamani ya shilingi milioni 700 utapunguza ukataji miti na kulinda hifadhi kwa kutumia raslimali kwa busara zaidi.

Mradi huo unatarajiwa kuwezesha wananchi wa maeneo hayo kupunguza umaskini kwa kutumia raslimali zilizopo kwa busara na wakati huo huo kuhifadhi mazingira.
DSC_0012
Afisa Mradi wa uchumi wa kijani ndani ya hifadhi hai (GEBR) Kitengo cha Sayansi kutoka UNESCO na mwakilishi wa KOICA, Myoung Su Ko, akisaini kitabu cha wageni kwenye ofisi za kata ya Mnyuzi mara baada ya kuwasili wilayani hapo kwa ajili ya kuzindua mradi wa mamilioni katika eneo la hifadhi Usambara Mashariki, na kuendesha mafunzo kwa wakazi waliomo na wanaozunguka hifadhi ya Usambara Mashariki.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...