Waziri
wa Mambo ya Ndani ya Nchi, ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Nachingwea, Mathias
Chikawe (kushoto) na waombolezaji wakiswalia mwili wa marehemu ambaye ni mama
mzazi wa Diwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Nachingwea, Sada Makota. Mazishi ya Mama Mzazi wa Diwani
huyo yamefanyika katika Kijiji cha Nangunde, Kata ya Namikango wilayani
Nachingwea leo.
Waziri
wa Mambo ya Ndani ya Nchi, ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Nachingwea, Mathias
Chikawe (kulia) akimfariji Diwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Nachingwea, Sada
Makota kwa kufiwa na mama yake mzazi, wakati alipofika nyumbani kwa Diwani huyo
wakati wa shughuli za maziko yaliyofanyika katika Kijiji cha Nangunde, Kata ya
Namikango wilayani Nachingwea leo.
Waziri
wa Mambo ya Ndani ya Nchi, ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Nachingwea, Mathias
Chikawe, akisaini katika kitabu cha maombolezo ya Mama Mzazi wa Diwani wa
Halmashauri ya Wilaya ya Nachingwea, Sada Makota, wakati alipofika nyumbani kwa
Diwani huyo katika Kijiji cha Nangunde, Kata ya Namikango wilayani Nachingwea
leo.
Waziri
wa Mambo ya Ndani ya Nchi, ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Nachingwea, Mathias
Chikawe (aliyevaa Miwani) akiwa na waombolezaji wa msiba wa Mama Mzazi wa
Diwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Nachingwea, Sada Makota. Mazishi ya Mama
Mzazi wa Diwani huyo yamefanyika katika Kijiji cha Nangunde, Kata ya Namikango
wilayani Nachingwea leo. Picha zote na Felix
Mwagara wa WMNN.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...