Mgeni rasmi kwenye kikao kilichoambatana na mafunzo ya mfuko wa taifa wa bima ya afya mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Lindi Vijijini bi Oliver Vavunge,ambapo aliwataka wawakilishi wafanyakazi kuwakumbusha kutimiza wajibu ili maslai yaweze kuboreka sanjari na kusisitiza kuwa watambue NHIF ina msaada mkubwa kwao na kwetu kama waajiriwa hivyo watumishi wa sekta ya afya wana jukumu kubwa la kusimamia huduma ili ziboreke zaidi kupitia fedha zinazolipwa kupitia bima ya afya,kushoto ni mwenyekiti Talgwu mkoa wa Lindi.
Washiriki wakimsikiliza kwa makini hayupo pichani meneja wa mfuko wa Taifa wa bima ya afya mkoa wa Lindi Bi Fortunata Raymond,ambapo aliweka bayana makusudio ya ofisi ya Mkoa wa Lindi ilivyoweka mkakati wa kutoa elimu inayohusu umuhimu na faida za kujiunga na mifuko ya afya ya jamii(CHF), sanjari na maboresho ya kitita cha mafao cha NHIF kwa viongozi wa vyama vya wafanyakazi mkoani Lindi.
katibu wa Kamati ya uratibu Talgwu Mkoa wa Lindi ndg kambogoro Rashidi akitoa  taarifa ya  madhumuni ya mkutano wa mwaka wa viongozi na kamati ya uratibu na utoaji wa elimu kutoka NHIF kwa mgeni rasmi ambaye ni Mkurugenzi wa Halmashauri ya Lindi Vijijini Oliva Vavunge.
Meneja wa mfuko mkoa wa Lindi Fortunata Raymond akifafanua jambo kwa mgeni rasmi ambaye ni Mkurugenzi wa Halmashauri ya Lindi Vijijini Bi Oliva Vavunge wa pili kulia..
 Meneja wa mfuko wa taifa wa bima ya afya mkoa wa Lindi Fortunata Raymond,akitoa elimu kwa viongozi na wawakilishi wa Talgwu ngazi ya kata na mkoa,kuhusu faida za kuwa mwanachama wa NHIF na mfuko wa afya ya jamii CHF kwenye ukumbi wa kanisa katoliki la Mt. Francisi Axvery mkoani Lindi Jana

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...