Ndugu zangu wanaDMV, nilikuja kwenu rasmi nikiomba kura zenu.Nia yangu ikiwa ni kuungana nanyi katika kutafuta njia za kutatua changamoto zinazotukabili hapa ugenini.
Malengo niliyo nayo kwa jumuiya hii na kwa jamii kwa ujumla sio malengo ya mpito.
Sisi wanaDiaspora tumeaacha nchi yetu nzuri, wazazi,watoto, ndugu hata marafiki kwa nia ya kuja kutafuta ahueni ya maisha.Maumivu na changamoto za ugenini ni sababu tosha za kutoruhusu jambo lolote kupotosha malengo yetu.
Nipo pamoja nanyi kama mgombea asiyefungamana na upande wowote, na nitaendelea kuwa nanyi licha ya matokeo ya Uchaguzi wa Viongozi wa Jumuiya ya WaTanzania, District of Columbia, Maryland and Virginia 2014.
Asanteni sana.
Harriet Shangarai
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...