MWL.ERNEST MWAMKAI KIONDO
1932-2014

Familia ya Mwl.Ernest Mwamkai Kiondo ya Dar es Salaam, Ambanguru, Mlalo, Korogwe  na kwaminchi Tanga .

Kwa  heshima na taadhima kuu tunapenda kutoa shukran zetu za dhati kwa ndugu,majirani, jamaa na marafiki  wote  ambao kwa namna moja au nyingine  waliweza  kushiriki katika msiba, wa Baba yetu mpendwa  aliefariki  Tarehe 22 May 2014 katika Hospital ya TCHC ,Tanga (TANGA CENTRAL HEAKTH CENTER) na kuzikwa  katika makaburi ya Bombo ,Tanga Tarehe 25 May 2014.  

Tumefarijika sana  pia kwa wale wakiosafiri  masafa marefu toka sehemu mbali mbali Nchini na nje ya Nchi  walitupa moyo wa Upendo tulipokuwa nao na faraja nyingi  tulizipata toka kwa watu mbali mbali waliotuma salaam za rambirambi toka sehemu mbali mbali duniani.

Haitakuwa rahisi kwetu kuwataja na kuwashukuru kila mmoja wenu  ingawa  tulipenda sana iwe hivyo, tunaomba kwa tangazo hili wote mtukubalie na mpokee  shukrani  zetu za upendo toka kwetu.
Hata hivyo familia inapenda kutoa shukran za pekee kwa waliochangia kutoa Huduma ambayo milele itabaki katika nyoyo zetu ,nao ni madaktari na manesi wa hospitali ya TCHC hususan DR.Gila na DR.Patrick kwa jitihada zao kuu za kumtibu baba yetu mpendwa.

Pia  tunapenda kuwashukuru wanajumuiya wote wa kanisa la nguvumali la Mtakatifu Yohana krisostomom  wa Nguvumali ,Tanga ,Baba Askofu Mahimbo  William Mndolwa alieongoza  misa  ya mazishi hayo na Padre kiongozi wa kanisa Isack  Nogea, Baba wa kiroho wa baba yetu na Father Paulo lihinga. Tunawashukuru sana .

Pia tunawashukuru viongozi wote wa mkoa wa Tanga uliongozwa na Katibu Tawala wa Mkoa ndugu Salum M. Chiwa kwa kushirikiana nasi katika msiba huo.

Mwisho tunapenda kuwajulisha kuwa tutahitimisha msiba wa baba yetu kwa kukesha nyumbani kwake Kwaminchi mjini Tanga siku ya ijumaa Tarehe  4 july 2014 na kufuatiwa na misa jumamosi  tarehe  5 july 2014 saa tano asubuhi katika kanisa la mtakatifu Yohana krisostomom, Nguvumali,Tanga.Wote mnakaribishwa 

Asanteni  sana.
BWANA AMETOA NA BWANA AMETWAA JINA LA BWANA  LIHIMIDIWE.
AMEN

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...