Ujumbe
kutoka Tanzania ukiwa Chuo Kikuu cha Calgary katika jimbo la Alberta nchini
Canada.Katika picha kutoka kushoto ni, Naibu Waziri wa Nishati na Madini,
Charles Kitwanga (wa saba), Naibu Waziri TAMISEMI, Kassim Majaliwa (wa tano),
Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais-Mazingira, Ummy Mwalimu (wa sita).
Wabunge, Richard Ndasa (wa nne), Deogratias Ntukamazina (wa tatu), Murtaza
Mangungu (wa pili) na Shafin Sumar (wa
kwanza kushoto. Wengine (kulia) ni wataalam kutoka Wizara ya Nishati na Madini
na watendaji kutoka Chuo Kikuu cha Calgary, Canada.
Ujumbe
kutoka Tanzania ukiwa katika makao makuu ya Taasisi ya Udhibiti Nishati katika
jimbo la Alberta nchini Canada.Katika picha ni, Naibu Waziri wa Nishati na
Madini, Charles Kitwanga (wa sita kutoka kulia), Naibu Waziri TAMISEMI, Kassim
Majaliwa (wa tano kutoka kulia), Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa
Rais-Mazingira, Ummy Mwalimu (wa tatu kushoto). Wabunge, Richard Ndasa (wa nne
kutoka kulia), Raya Khamisi (wa pili kutoka kulia). Wengine ni wataalam kutoka
Wizara ya Nishati na Madini na watendaji kutoka Mamlaka ya Udhibiti Nishati ya
Alberta wakiongozwa na Zeeshan Syed, Mkurugenzi wa Mahusiano ya Kitaifa,
Kimataifa na Serikali, (wa tatu kutoka kushoto).
============ ========= =========
Serikali yashauriwa kuwabana wawekezaji.
Serikali
ya Tanzania imeshauriwa kuweka sheria madhubuti zitakazohakikisha wawekezaji wa
kigeni wanaleta faida katika nchi badala ya kunufaisha makampuni yao tu.
Hayo
yamesemwa na Bw. Zeeshan Syed, Mkurugenzi wa Mahusiano ya Kitaifa, Kimataifa na
Serikali katika Taasisi ya Udhibiti Maendeleo ya Nishati ya Jimbo la Alberta
nchini Canada wakati alipokuwa akizungumza na ujumbe wa Tanzania ulioongozwa na
Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Charles Kitwanga uliofika katika makao makuu
ya Taasisi hiyo ikiwa ni sehemu ya ziara ya mafunzo kuhusu sekta ya uziduaji.
“kwa
kawaida wananchi huwa wana matarajio makubwa ya manufaa ya rasilimali
zinazowazunguka hivyo ni muhimu kwa serikali kuwa na sheria zitakazowabana
wawekezaji ili wanapomaliza shughuli zao, pia faida ibaki kwa wananchi” Alisema
Bw.Syed.
Mkurugenzi
huyo alieleza kuwa licha ya taasisi hiyo kuwa mdhibiti wa nishati lakini pia
ina jukumu la kudhibiti uhifadhi wa mazingira ili kuhakikisha kuwa shughuli za uendelezaji
wa nishati zinafuata sheria za nchi za utunzaji mazingira.
Naye
Naibu Waziri wa Nishati na Madini anayeshughulikia Nishati, Charles Kitwanga
alimweleza Bw.Syed kuwa licha ya Tanzania kuwa na Mamlaka ya Udhibiti wa
Nishati na Maji (EWURA) lakini bado nchi inahitaji kujifunza kutoka kwa nchi
nyingine zenye uzoefu ili kuboresha shughuli za udhibiti nchini Tanzania.
“Shughuli
za udhibiti nishati katika Taasisi hii zina zaidi ya miaka 75 na hivyo Tanzania
inahitaji kupata uzoefu kutoka kwenu ili kufahamu hatua mlizopitia kufika hapa
mlipo leo”. Alisema Waziri Kitwanga.
Wakati
huohuo Naibu Waziri na ujumbe wake unaojumuisha baadhi ya wabunge kutoka Kamati
ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini walitembelea Chuo Kikuu cha Calgary
ambacho kimebobea katika kutoa elimu juu ya masuala ya sera za Uchumi, Nishati,
Mazingira na kutoa ushauri katika utengenezaji sera katika sekta ya uziduaji.
Katika
Chuo hicho ujumbe huo ulikutana na Mkurugenzi anayeshughulikia Sera za Umma, Bw.Jack
Mintz ambaye aliueleza ujumbe huo kuwa Tanzania ni moja
kati ya nchi sita duniani (huku ikiwa ni pekee kutoka Afrika) ambazo zinapewa
kipaumbele na chuo hicho katika masuala ya ushirikiano wa kujenga uwezo kwenye
masuala ya sera.
Mkurugenzi
huyo alieleza kuwa, Chuo cha Calgary pia kitashirikiana na Tanzania katika kuwajengea
uwezo watumishi kwa kutumia pia vyuo vingine ambavyo wana ushirikiano navyo na
kwamba mafunzo hayo yanaweza kufanyika ndani na nje ya Tanzania .
Pamoja
na suala la kujenga uwezo kwa watanzania ili kuweza kuandaa sera zitakazokuwa
na manufaa kwa nchi Bw.Mintz aliueleza ujumbe huo kuwa ni muhimu kwa serikali
ikawa ndiyo msimamizi mkuu wa rasilimali za nchi ili faida zinazotokana na rasilimali
hizo ziwafikie wananch wote.
Naye
Naibu Waziri Katika Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
(TAMISEMI), Kassim Majaliwa pamoja na kushukuru kwa Tanzania kupewa kipaumbele na
Chuo hicho katika kujenga uelewa, alimweleza Mkurugenzi huyo wa Chuo kuwa
Tanzania kwa sasa inakaribisha wawekezaji wa ndani na nje kuwekeza Tanzania hivyo
suala la kupata elimu na uzoefu zaidi ili kuendana na kasi ya uwekezaji linapewa
kipaumbele.
Ukiona competitor wako anakuwa mshauri wako, basi umeliwa saaaaaaaaaaana!
ReplyDelete