Mfuko wa Maendeleo ya Jamii TASAF umeajiri Wataalamu waelekezi ( TA) ambao watatoa huduma katika halmashauri mbalimbali nchini kwa lengo la kusimamia ipasavyo shughuli za Mpango wa kunusuru kaya masikini na zinazoishi kwenye mazingira hatarishi PSSN.Watalaam waelekezi hao wako katika mafunzo kwenye ukumbi wa CEEMI jijini Dar es salaam.
 Mkurugenzi Mtendaji wa Mfuko wa Maendeleo ya Jamii TASAF ,Ladislaus Mwamanga (wa nne kutoka kushoto) akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya Wataalam Waelekezi wapya (TA)ambao wako katika mafunzo ya namna ya utekeleza majukumu yao katika Mpango wa Kunusuru Kaya masikini PSSN ulioko chini ya TASAF awamu ya TATU. Walioketi ni baadhi ya wakurugenzi na mameneja wa TASAF.

Mkurugenzi  Mtendaji wa Mfuko wa Maendeleo ya Jamii TASAF ,Ladislaus Mwamanga (aliyesimama) akitoa hutuba ya ufunguzi wa mafunzi ya Wataalam Waelekezi (TA) walioajiriwa na TASAF kwa ajili ya kuhudumia Halmashauri za wilaya mbalimbali nchini (hawapo pichani)ikiwa ni mkakati wa kufanmikisha Mpango wa kunusuru kaya masikini nchini.
 Baadhi ya wataalamu Waelekezi TA wapya walioajiriwa na Mfuko wa Maendeleo ya Jamii TASAF wakisikiliza hoyuba ya ufunguzi wa mafunzo yao katika ukumbi wa CEEMI ambayo ilitolewa na Mkurugenzi Mtendaji wa TASAF ,Ladislaus Mwamanga hayupo pichani  ambaye pamoja na mambo mengine alisistiza umuhimu wa wataalamu hao kufanya kmazi kwa uaminifu na kujituma na kushirikisha sekta nyingine kwenye halmashauri watakazopangiwa.
 Baadhi ya Wataalam waelekezi  wapya (TA ) watakaotoa huduma katika halmashauri mbalimbali nchini wakimsikiliza Mkurugenzi Mtendaji wa TASAF Bwana Ladislaus Mwamanga hayupo pichani wakati alipofungua mafunzo elekezi ya namna ya kutekeleza majukumu yao kikamilifu kwa lengo la kufranikisha Mpango wa Kunusuru Kaya masikini nchini,PSSN.
 Meneja Rasilimali watu wa Mfuko wa Maendeleo ya Jamii TASAF Bi Thecla  Makundi (aliyeshika tama)akimsikiliza kwa makini mmoja wa Wataalamu Waelekezi wapya alipokuwa akitoa maelezo katika mafunzo ya watalaam hao yanayofanyika kwenye ukumbi wa CEEMI jijini DSM.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...