Mbunge wa jimbo la Kilolo Prof. Peter Msola akizungumza na wananchi wa
kijiji cha Mwatasi katika kata ya Bomalang'ombe katika jimbo la Kilolo
wilayani Kilolo Mkoani Iringa.
baadhi ya wakazi wa kijiji cha Mwatasi waliohudhuria mkutano wa hadhara katika kiwanja cha shule ya msingi Mwatasi wakisikiliza hotuba ya mbunge wao Prof Peter Msola
Mmoja wa wakazi wa jimbo la Kilolo, Ayubu Sanga akitoa taarifa ya kijiji cha Mwatasi mbele ya Mbunge wa jimbo hilo Prof. Peter Msola
baadhi ya wakazi wa kijiji cha Mwatasi waliohudhuria mkutano wa hadhara katika kiwanja cha shule ya msingi Mwatasi wakisikiliza hotuba ya mbunge wao Prof Peter Msola
Mmoja wa wakazi wa jimbo la Kilolo, Ayubu Sanga akitoa taarifa ya kijiji cha Mwatasi mbele ya Mbunge wa jimbo hilo Prof. Peter Msola
-============
Na Denis
Mlowe, Kilolo
MBUNGE wa
jimbo Kilolo, Profesa Peter Msola amewataka wananchi wa jimbo hilo kuwekeza
katika elimu kwa kuwapeleka watoto wanaotakiwa kuanza shule na kuondokana na
janga la kukosa elimu katika wilaya hiyo.
Profesa Msola
aliyasema hayo wakati akizungumza na wananchi wa Jimbo la Kilolo katika kijiji
cha Mwatasi kata ya Bomalang’ombe wakati wa ziara ya siku moja kwa wananchi wa
jimbo hilo juzi na kusisitiza umuhimu wa wazazi kuwaelimisha na kuwapatia elimu
watoto wao.
Msola alisema
kuna wazazi ambao wanashindwa kuwekeza katika elimu na kuwafanya watoto wao
kukimbilia mijini ambapo maisha ya huko ni magumu bila kuwa na elimu na
kuwataka kukazania elimu kwa watoto wao kwanza.
Alisema kuwa
maendeleo miongoni mwa jamii
yanachangiwa kwa kiasi kikubwa na kiwango cha uwekezaji katika elimu, ni vema
jamii iwekeze kwa kiwango kikubwa katika sekta ya elimu ili kujikwamua na
umaskini uliopo na kupambana katika soko la ajira.
“Tukumbuke
kwamba kuwekeza katika elimu ni mkakati wa muda mrefu unaohitaji dhamira,
subira na kwamba matokeo yake huonekana baada ya muda mrefu wa uwekezaji na
faida kwa wazazi mara baada ya mtoto kusoma na kuweza kumsaidia pindi azeekapo”
alisema Prof. Msola
Aidha Prof
Msola alisema wilaya ya Kilolo ina rasilimali nyingi zinazohitaji viongozi
wabunifu watakaohakikisha zinatumiwa vizuri kwa faida ya watu wote hivyo bila
kuwekeza katika elimu rasimali hizo zitatumiwa vibaya na watu wasiojua faida ya
elimu.
Aliongeza kuwa
katika mipango yake ya kuifikisha wilaya
hiyo kwenye kilele cha mafanikio, atahakikisha barabara zinazotakiwa
kuiunganisha wilaya hiyo na wilaya nyingine zaidi zinajengwa.
Alisema
hatua hiyo itaongeza shughuli za uwekezaji, utalii, kilimo na biashara na hivyo
kuwaongezea kipato wananchi wake.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...