Maafisa wa Ubalozi, Bwana Amos Msanjila na Dada Caroline Chipeta, Wakimkaribisha Mheshimiwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano, Mhe. Mizengo Pinda na Mkewe (Mama Tunu Pinda) walipowasili katika Ofisi za Ubalozi wa Tanzania, London
 Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano, Mhe. Mizengo Peter Pinda akipokewa, kukaribishwa na kusalimiana na baadhi ya Maafisa wa Ubalozi pamoja na Wawakilishi wa Jumuiya za Watanzania waishio nchini Uingereza.

 Baadhi ya Watanzania waliohudhuria Mkutano wao na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania.

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,  Mhe. Mizengo Pinda, alikutana na kuzungumza na Watanzania wanaoishi nchini Uingereza siku ya Jumamosi tarehe 12 Julai 2014, mara baada ya ziara yake fupi ya kikazi nchini humo.

Mkutano huo na Watanzania ambao uliofanyika Ubalozini, Mheshimiwa Waziri Mkuu alitoa taarifa mbalimbali za maendeleo nchini, hususan mchakato wa Katiba mpya, sera ya Diaspora na maandalizi ya chaguzi mbalimbali zinazokuja. 
Mkutano huo ulimalizika kwa maswali na majibu na baadae wananchi kupiga picha na Waziri Mkuu kama inavyoonekana kwenye picha hizi hapo chini.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...