MWIGIZAJI wa kike wa filamu Aisha Bui, amedai kuwa alijitoa maisha yake kutoka na filamu yake ya Mshale wa Kifo, kutokana na sinema hiyo kutengeneza porini katika msitu hatari wenye wanyama wakali.

Msanii huyo amedai alifanya hivyo kufuatia maoni ya wapenzi wa filamu ambao kila siku wanalalamika kwa kusema kuwa filamu zetu nyingi zimekuwa za mijini tu, huku baadhi ya matukio yakirudiwa kila katika sinema hizo jambo ambalo limekuwa likiongelewa mara kwa mara.

“Nilijitoa maisha yangu kwa kuingia msituni kutengeneza filamu ya mapigano porini, kutafuta uhalisia, lakini najua na deni kwa wapenzi wa kazi zangu, wanajua kuwa mimi ni bora hivyo lazima niwe bora kila mwaka,”anasema Asha .

Filamu ya Mshale wa Kifo Imetengenezwa na Yuneda Entertainment na imewashirikisha wasanii nyota kama Ahmed Olotu ‘Mzee Chilo’, Asha Bui, Salim Ahmed ‘Gabo Zigamba’ na wasanii wengine

Sinema hiyo imerekodiwa Mkoani Morogoro Vijijini ikiwa ni hatua nyingine kwa watayarishaji wa filamu kwenda kucheza filamu nje ya jiji la Dar es Salaam kama ilivyozoeleka, Aisha anasema kuwa maeneo yanayotumika yanarudiwa sana hata baadhi ya watazamaji wameyashika kwani yanaonekana kila filamu.

Aisha Bui akiwa Salim Ahmed ‘Gabo Zigamba’ katika moja ya scene za filamu ya Mshale wa Kifo.

Aisha akiwa yupo porini na msanii mwenzake Gabo wakiendelea kurekodi filamu ya Mshale wa Kifo katika misitu ya Morogoro.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...