Idara ya
Uhamiaji nchini imewakamata raia wanane wa kigeni (pichani
chini) wakati wakiingia nchini kupitia Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu
Nyerere wakiwa na pasipoti bandia za kusafiria za Mataifa
tofauti ya Ulaya.
Wageni hao
walikuwa wakijaribu kuingia nchini leo tarehe 15.08.2014 majira ya saa nane na
nusu usiku kwa ndege ya shirika la ndege la Uturuki yenye
Namba TK 603, wakitokea Uturuki na kujitambulisha kuwa ni raia
wa Sweden na Belgium.
Maofisa Uhamiaji katika kituo hicho baada ya kuwatilia mashaka na
kuwafanyia ukaguzi wa kina, waligundua kuwa wageni hao ni Raia wa Iraq
wakijaribu kuingia nchini Tanzania na pasipoti za bandia.
Kukamatwa kwa wageni hao ni jitihada za Idara ya Uhamiaji kupambana na
Uhamiaji haramu nchini ambapo suala la zima la udhibiti wa mipaka linapewa
kipaumbele.
Akizungumzia tukio hilo, Kaimu
Msemaji Mkuu wa Idara ya Uhamiaji Tatu Burhan, anasema, kwa kutumia ujuzi
na weledi walionao Maofisa Uhamiaji wanaendelea kufanyakazi usiku na machana
kuhakikisha Sheria na Taratibu za Uhamiaji zinafuatwa.
"Idara ya Uhamiaji, iko macho hatulali ili kuhakikisha ulinzi
na usalama wa nchi ikiwa ndio jukumu letu namba moja unaimarika. kwahivyo,
kila mtu awe raia wa kigeni na Watanzania wanapaswa kufuata Sheria na
Taratibu zilizopo za kuingia na kutoka nchini"
Hadi sasa, Wageni hao wamezuiliwa
kuingia nchini na wanaendelea kushikiliwa na Maofisa wa Idara ya Uhamiaji
kituoni hapo huku wakisubiri kurudishwa walikotoka.
Hili ni wimbi lilioibuika hivi karibuni kwa baadhi ya raia wa nchi za
Iraq, Iran, Syria kujaribu kuingia nchini isivyo halali huku ikisemekana lengo
lao kubwa ni kuingia Tanzania na baadae kutoka kuelekea mataifa ya Ulaya.
Majina ya Wageni hao na Pasipoti bandia
walizokuwa wakitumia pamoja na Majina halisi na Pasipoti zao za
Iraq zilizogunduliwa baada ya upekuzi kwenye mabano ni kama ifuatavyo;
1. ADEL SHAALAN MOHAN - SWEDISH, PPT. NO.
EI282207 ( ADEL SHAALAN MOHAN Pasipoti Nam. G1489664)
2. SAMER HELMI KAMIT -
SWEDISH, PPT. NO. 87187804 ( LAZIM MOSA HITEET, PPT. Namba, A 13466001)
3. MOHAMMED JAFAR AL MOSAWI - SWEDISH, PPT.NO. 87168871 (ALI HUSSEIN OLEIWI, PPT. NO.
G 1111623)
4. DAVID GABRIEL POBLETE -
SWEDISH PPT.NO. 86867751 (AYAD SAMI MAKTTOOF, PPT NO.
A 4910203)
5. SADDAM ALKHAMERI AREF - SWEDISH,
PPT NO. 81640513 (SAIF ALDAN FALIH HASAN, PPT. NO. G 1489664)
6. ALI MOHAMMED ABDULLAH - IRAQ, PPT. NO. A 5931725
7. OSAMAH ZAID GHAEB AL-OBAIDI - IRAQ, PPT. NO. A
6175951
8. ALI HUSSEIN OLEIWI - IRAQ, PPT. NO. G
1111623
Uhamiaji endeleza kazi hizi ili mchangie ulinzi wa mipaka ya nchi hii kama mnavyotarajiwa kufanya.
ReplyDeletewahusika wa uhamiaji swala la wahamiaji wanaotokea nchi zenye hali ya machafuko ya usalama kama Gaza-Palestine na Iraq ni swala la kimataifa tusiwachukulie wote
ReplyDeletekama wahamiaji haramu yawezekana
umoja wa taifa umechangia kuwasaidia vyeti vya usafiri walivyonavyo kutokana na hali halisi ya mauaji yasiyo na msingi zidi ya tofauti za dini na siasa.
Tanzania chini ya uongozi wa awamu ya kwanza baba wa Taifa na serikali walifanya maamuzi magumu ya kuwapatia hati za usafiri za Tanzania viongozi wa Frelimo na South Africa kumbukumbu rudieni
hotuba ya raisi Jakaya Kikwete akiwepo South Africa kuhusu matumizi ya hati za Tanzania kwa raisi mstahafu Tabu Mbeki na wengine.Tanzania tuendelee kuwa wavumilivu na wahamiaji wa nchi zenye machafuko.Palestine na Iraq ni marafiki zetu sawa wachina na wahindi.wapewe ushauri,misaada ya kimataifa kama hawana nia mbaya.
MIKIDADI-DENMARK
Great work by Immiigration really deserve the credits to intercept and cupture those Illegals because who knows as to why they were trying to inter the country with false identity? But the great job doesn't end there. They should continue to dig deeper to find out the really identity of those 8 illegals and the reason why they ware trying to infiltrate our country. They could be Terorrists
ReplyDeleteKwanini Tanzania????Je yawezekana kuna wenzao waliofanikiwa awali??Ni dhahiri si mpango mdogo.......tuwe macho zaidi si hapo tu.....huko mipakani ndio usiseme......kwakua hatutumii satelite wa...........
ReplyDeleteHuenda wana uraia wa kupewa toka Sweden sababu ya ukimbizi na wamekuja tafuta uwekezaji bongo,pale sweden wanawapa hao uraia Sababu kwao kuna vita
ReplyDeleteHata kama nchi zao zina hali ngumu suala Zima linabakia kuwa KWA NINI WAGUSHI NYARAKA!!!? Ni bora wangejisalimisha kama wakimbizi basi halafu uhamiaji ijue cha kufanya.
ReplyDeleteHivi vitambulisho vya taifa viko wapi jamani? Haiwezekani waje hivi hivi, ina maana kuna wenzao tayari wameshafanikiwa kuingia kilaini. Msako mkali ufanyike kuwabaini ambao tayari wamo nchini.
Ni kazi nzuri na ya kuonyesha umakini kwa idara ya Uhamiaji.
ReplyDeleteLakini wote tumesahau kuwa hawa raia pengine wana uraia wa nchi mbili na walitaka kwenda mahala.
Uchunguzi uwe ni kubaini kama wana uraia pacha na lini kusudio la safari yao.
Iraq inarusu uraia wa nchi mbili. Hivyo kuwa na passport zao za asili, isiwe sababu ya kuwa wahamiaji haramu.
ReplyDeleteWatatuletea vita.Warudisheni kwao
ReplyDelete