Rais Jakaya Mrisho Kikwete,  Makamu wa Rais Dkt Mohamed Gharib Bilali, Waziri Mkuu Mhe Mizengo Pinda,  Waziri wa Sheria na Katiba Dkt Asha-Rose Migiro, Jaji Mkuu wa Tanzania Mhe Mohamed Chande Othman, Jaji Mkuu wa Zanzibar Mhe Omar Othman Makungu,  Katibu Mkuu Kiongozi  Balozi Ombeni Sefue, Mwanasheria Mkuu Jaji  Frederick Werema, Mtendaji Mkuu wa Mahakama Mhe Hussein kattanga  katika picha ya pamoja na Majaji wa Mahakama kuu ya Tanzania baada ya kuapishwa leo Ikulu jijini Dar es salaam.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete  akiwa na Jaji Mkuu wa Tanzania Mhe Mohamed Chande Othman, Jaji Mkuu wa Zanzibar Mhe Omar Othman Makungu pamoja na  Majaji wa Mahakama ya Rufaa Tanzania na Majaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania wapya
 Rais Jakaya Mrisho Kikwete  akiwa na Jaji Mkuu wa Tanzania Mhe Mohamed Chande Othman, Jaji Mkuu wa Zanzibar Mhe Omar Othman Makungu pamoja na  Majaji wa Mahakama ya Kuu Tanzania na Majaji  wapya
 Rais Jakaya Mrisho Kikwete  akiwa na Jaji Mkuu wa Tanzania Mhe Mohamed Chande Othman, Jaji Mkuu wa Zanzibar Mhe Omar Othman Makungu pamoja na  majaji wapya 
  Jaji Mkuu wa Tanzania Mhe Mohamed Chande Othman, Jaji Mkuu wa Zanzibar Mhe Omar Othman Makungu na Jaji Kiongozi   Shaban Ally Lila wakiwa na Majaji wapya 
 Rais Kikwete na Waziri wa Sheria na Katiba Dkt Asha Rose Migiro wakiwa wa wanachama wa Chama cha Wanasheria Wanawake (TAWLA) na Majaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania wanawake wapya
  Rais Jakaya Mrisho Kikwete, Jaji Mkuu wa Tanzania Mhe Mohamed Chande Othman, Jaji Mkuu wa Zanzibar Mhe Omar Othman Makungu na Jaji Kiongozi   Shaban Ally Lila wakiwa katika pic ha ya jumla na Majaji wapya na wa zamani. Kwa picha zaidi BOFYA HAPA

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete asubuhi ya leo, Ijumaa, Agosti 15, 2014, amewaapisha Majaji 20 wapya wa Mahakama Kuu ya Tanzania ambao aliwateua mwanzoni mwa wiki hii katika hafla iliyofanyika Ikulu, Dar Es Salaam.
Halfa hiyo iliyofanyika Ikulu, Dar Es Salaam ilihudhuriwa pia na Makamu wa Rais Mheshimiwa Mohamed Gharib Bilal,  Waziri Mkuu Mheshimiwa Mizengo Pinda, Jaji Mkuu wa Tanzania Mheshimiwa Mohamed Chande Othman, Waziri wa Katiba na Sheria Mheshimiwa Asha Rose Migiro na Jaji Mkuu wa Zanzibar Mheshimiwa Omar Othman Makungu.
Majaji hao wapya wa Mahakama Kuu ya Tanzania ni pamoja na akinamana wanane na uteuzi huo wa Mheshimiwa Rais Kikwete umeshirikisha wanasheria kutoka Serikalini, Taasisi za Umma, Jumuia ya Afrika Mashariki, Sekta Binafsi na Asasi za Kiraia.
Majaji hao wapya ambao wameapishwa leo ni Jaji Penterine Muliisa Kente, Jaji Benedict Batholomew  Mwingwa,  Jaji Eliezer Mbuki Feleshi, Jaji John Eudes Ruhangisa, Jaji Winfrida Beatrice Korosso, Jaji Lilian Leonard Mashaka, Jaji David Eliad Mrango, Jaji Edson James Mkasimongwa, Jaji Mohamed Rashid Gwae na Jaji Firmin Nyanda Matogoro.
Wengine ni Jaji Leila Edith Mgonya, Jaji Barke Mbaraka Abdou Sehel, Jaji Awadhi Mohamed, Jaji Lugano J. Mwandambo, Jaji Rose Ally Ibrahim, Jaji Paul Kihwelu, Jaji Modesta Opiyo Makopolo, Jaji Amour Said Khamisi, Jaji Mary Caroline Levira na Jaji Salma Maghimbi.
Imetolewa na:
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu.
Dar es Salaam.

15 Agosti, 2014



Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...