KIKUNDI cha Ngoma za asili cha Bujora cha jijini Mwanza kimefanikiwa kuchukua ubingwa wa fainali za mashindano ya Ngoma za asili kanda ya ziwa mwishoni mwa wiki kwa pointi 87.5 zilizofanyika katika Uwanja wa Mabatini kwa kushirikisha mabingwa wawili kutoa katika mikoa mitano ambayo ni Tabora, Shinyanga, Kagera,Mara na Mwanza.

Kwa ubingwa huo kikundi cha Bujora kilizawadiwa pesa taslimu shilingi 1,100,000/= , kikombe pamoja na medali za dhahabui cha Mwanalyaku ambao walipata pointi .

Nafasi ya Pili katika fainali hizo ilichukuliwa na kikund Mwanalyaku cha jijini Mwanza pia kwa pointi 79.5 na hivyo kuzawadiwa pesa taslimu shilingi 850,000/=, Nafasi ya tatu ilichukuliwa na kikundi cha Bugoloile cha Kagera kwa pointi 79.3 na hivyo kuzawadiwa pesa taslimu Shilingi 600,000/=.Nafasi ya nne ilikwenda kwa kikundi cha Mabulo ya Jeshi cha Sinyanga kwa pointi 76.7 na hivyo kuzawadiwa pesa taslimu Shilingi 500,000/=.

Nafasi ya tano mpaka ya kumi ni kikundi cha Rugu kagera pointi 75.2,Musoma One cha Mara 73.8,Wanunguli Shinyanga pointi 73.1,Magereza Tabora 70.1,Kiwajaki Mara 69.6 na cha mwisho ni kikundi cha Bugobogobo cha Tabora pointi 59.3.

Mgeni rasmi katika fainali hizo alikuwa Kaimu Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Mwanza, Christopher Fuime ambaye aliishukuru Kampuni ya Bia Tanzania kwa kuzamini mashindano ya ngoma ambayo hufanyika kila mwaka wakati wa mavuno ambapo aliwaomba waendelee kudhamini kwani yanatukumbusha asili yetu tulikotoka na pia zawadi wanazopata zinaongeza kipatao kwa washiriki.

Nae Meneja wa Bia ya Balimi Extra Lager, Edithi Bebwa aliwashukuru washiriki wote kwa kuwa mabingwa wa mkoa yao huko wanakotoka na pia aliwashukuru kwa kushiriki fainali za Kanda na kuwaahidi kuboresha zaidi mashindano mwaka ujao hasa upande wa zawadi.

Edithi alisema sababu msinigi ya kuwepo kwa Mashindano ya Balimi Ngoma za Asili ni kuenzi na kulinda utamaduni wa Kitanzania. Kampuni ya Bia nchini ni sehemu yao ya kurudisha fadhila kwa watumiaji wa Kinywaji cha Balimi Extra Lager pamoja na vinywaji vyote vya Kampuni ya Bia Tanzania(TBL).
Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Christopher Fuime(kulia) akimkabidhi kikombe kiongozi wa kikundi cha ngoma cha Bujora mara baada ya kuibuka mabingwa wa Kanda ya Ziwa wa fainali za mashindano ya Ngoma za Asili yalifanyika katika Uwanja wa Mabatini jijini Mwanza mwishoni mwa wiki.
Baadhi ya wacheza ngoma wa kikundi cha Bujora wakishangilia na kikombe pamoja na pesa taslimu shilingi 1,100,000/= mara baada ya kuibuka mabingwa wa Kanda ya Ziwa wa fainali za mashindano ya Ngoma za Asili yalifanyika katika Uwanja wa Mabatini jijini Mwanza mwishoni mwa wiki.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...