Mkurugenzi Mkuu wa Drive Dentsu, Mr Cheriff
Tabet (kushoto)akizungumza na waandishi wa habari wakati wa uzinduzi wa ofisi
yao Dar es Salaam. Kulia kwake ni Meneja Uendelezaji wa Biashara na Masoko
Mapya, Rami
El Khalil.
Mkurugenzi Mkuu wa Drive Dentsu, Mr Cheriff
Tabet (katikati)akizungumza na waandishi wa habari wakati wa uzinduzi wa ofisi
yao Dar es Salaam. Kulia kwake ni Meneja Uendelezaji wa Biashara na Masoko
Mapya, Rami
El Khalil, na kushoto ni Meneja Mkuu wa Drive Dentsu Tanzania, Terry Greenwood.
======== ======== =========
Dar es Salaam, 26-August, 2014: Kampuni ya Drive
Dentsu, imefungua ofisi zake mpya jijini Dar es Salaam katika jitihada za
kusogeza huduma zake kwa wateja wake katika ukanda wa Afrika Mashariki.
Ikiwa ni kampuni
iliyotanda nchi zaidi ya 110, Drive Dentsu ni sehemu ya muunganiko wa kimataifa
wenye zaidi ya wafanyakazi 37000 na ofisi 160 duniani kote, muunganiko ambao unaleta
pamoja ujuzi, maarifa na vitendea kazi vyenye kuhakikisha inawapa wateja wake
huduma zenye ubora wa hali ya juu.
Akiongea na
waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, Bw. Cheriff Tabet, Mkurugenzi Mkuu wa
Drive Dentsu, amesema ufunguzi wa ofisi mpya ya Drive Dentsu jijini Dar unalenga
kutoa suluhisho la ubunifu kwa makampuni na bidhaa za kitanzania.
Bw. Tabet
amesema pamoja na kuwekeza nchini Tanzania, Drive Dentsu imelenga kujipanua
katika masoko mengine katika ukanda huu ili kuhakikisha wanakidhi mahitaji yao
kwa kutoa suluhu kwa changamoto zote za kibiashara.
“Katika ukanda wa Afrika Mashariki, uchumi wa
Tanzania umekua ukikua kwa kasi kubwa pamoja na ongezeko la uzalishaji wa bidhaa
nyingi jambo ambalo linakuza mazingira yenye ushindani hivyo kufanya kuwepo na uhitaji
mkubwa wa ubunifu katika kuwafikia wateja’ anasema Bwana Tabet.
Tabet pia
anasema kuwa Drive Dentsu inaleta uzoefu wake mkubwa, nchini Tanzania, ambao
umewawezesha kutwaa tuzo 17 za kimataifa
na kitaifa katika tasnia ya ubunifu wa matangazo. Naye Bw. Rami El
Khalil, Meneja Mkuu wa Masoko na Maendeleo ya Biashara wa Drive Dentsu anasema
Tanzania ni nchi yenye fursa nyingi kutokana na uchumi wake kuwa imara hivyo ni
sehemu nzuri kuwekeza.
‘Drive Dentsu
itaweka muhimili mpya katika tasnia hii ikiwa na mtazamo mpya wenye kusaidia
chapa kujidhihirisha na kutambulika kwa watumiaji wake’ anasema Bw. Rami. Pia Drive Dentsu
wamewekeza katika wataalam mahiri walioko nchini, hili linajidhirisha walipomteua
Terry Greenwood kuwa Meneja Mkuu wa kampuni hiyo nchini Tanzania.
Terry mwenye
uzoefu wa zaidi ya miaka 41 katika tasnia ya mawasiliano, amepata uzoefu huo katika
makampuni mbalimbali huko Amerika, China na Mashariki ya Kati. Pia kwa miaka
saba sasa amekuwa akifanya kazi na Drive Dentsu.
Kwa uzoefu wake
na ushirikiano kutoka kwa mtandao wa Drive Dentsu kimataifa tunaamini ataleta
mapinduzi katika tasnia ya utengenezaji matangazo. Wateja wa Drive
Dentsu kwa sasa ni kama Zantel, Moov, Moneygram, Radisson Royal Hotel,
Daihatsu, Hitachi, Jammal Trust Bank, Toshiba, Lexus, Bridgestone, Jumeirah dot
Shabaka, Toyota, Virgin, Abdul Latif Jameel na Vitaene C.
‘Ofisi zetu
nchini Tanzania zitakuwa ni sehemu ya kuimarisha muunganiko wetu kimataifa, pia
itaiwezesha Drive Dentsu kuwasaidia wateja wetu kukabiliana na mabadiliko ya
kila siku katika biashara’ anamaliza Bwana Rami.
Hii yanikumbusha atikali nyingi zinavyoonyesha ufundishaji wa uhadishi wa habari Bongo bado tuko mbali.
ReplyDeleteSasa mtu utaandika ahabari kuhusu kampuni bila kusema biashara gani wanajishughulisha nazo? umetaja wakuu wao, ukasema wana wafankyazi kadhaa, ukasema idaidi ya nchi waliko na ofisi, uka nakiri matamshi bioa kusema la msingi????
mara kwa mara utaoan wahandisha wanatuwekea picha za viongozi na habari chini ya picha " fulani akimwambia jambo???"
kazi ipo ndugu..wapigananaji kweli inatakiwa kukazi uzi..uhandishi wa habari kupasha na keulemisha..sasa Drive Dentsu ni mdudu gani..ndio tumeona meeneja na dk..
Drive Dentsu ni kampuni inashughulika na nini?
ReplyDeleteNaoana itabidi ku google.hi.kampuni maana kiukweli habari haikukamilika....
ReplyDelete