Mwenyekiti  wa Mfuko wa Fursa Sawa kwa Wote(EOTF), Mama Anna Mkapa akitoa neno la shukrani kwa wahisani wakati wa hafla ya kukabidhi  vitabu kwa ajili ya kusaidia  shule 45 na vyuo 3 vilivyotolewa na Books for Africa kutoka nchini  Marekani leo jijini Dar es Salaam,kushoto ni Mwakilishi kutoka Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Bibi.Paulina Mkonongo na katika ni mwakilishi wa Balozi wa Nigeria nchini Bibi. Abiola Delupe.
 Mkurugenzi Mtendaji wa Mfuko wa Fursa Sawa kwa Wote(EOTF), Emmanuel  Matee akielezea historia ya mfuko huo kwa wadau mbalimbali wa elimu katika hafla ya kupokea vitabu kwa ajili ya shule za Msingi, Sekondari na Elimu ya Juu vilivyotolewa na Books for Africa kutoka Marekani leo jijini Dar es Salaam
 Mwenyekiti  wa Mfuko wa Fursa Sawa kwa Wote (EOTF), Mama Anna Mkapa akimkabidhi kitabu mwakilishi wa Shule ya Sekondari Overland, iliyopo Kisarawe ndg. Allison Sila  wakati wa hafla ya kukabidhi  vitabu kwa ajili ya kusaidia  shule 45 na Vyuo 3 vya Elimu ya Juu vilivyotolewa na Books for Africa kutoka nchini  Marekani na kusafirishwa kwa hisani ya Mfuko wa Sir. Emeka Offod wa nchini Nigeria  leo jijini Dar es Salaam.

Mwenyekiti  wa Mfuko wa Fursa Sawa kwa Wote (EOTF), Mama Anna Mkapa akiwa katika picha ya pamoja na wadau pamoja na wahisani wa Elimu wakati wa hafla ya kukabidhi vitabu kwa ajili ya  kusaidia  shule 45 na Vyuo 3 vya Elimu ya Juu vilivyotolewa na Books for Africa kutoka nchini  Marekani na kusafirishwa kwa hisani ya Mfuko wa Sir. Emeka Offod wa nchini Nigeria leo jijini Dar es Salaam. Picha na MAELEZO

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...