Na Sultani Kipingo
Wengi tumesoma vitabu vya James Hadley Chase (pichani), mwandishi
wa riwaya za kusisimua maarufu sana wa
Uingereza, hasa wakati tukipambana na kujua lugha ya Kiingereza wakati wa shule
kidato cha kwanza hadi cha nne, na hata high school.
Nadhani kwa hili
hata Profesa Mbele ataniunga mkono ninaposema kuwa utamaduni wa kupenda kusoma
huanzia kwenye kuwepo kwa vitabu vya kusisimua kama vya Chase. Na wengi tuliua
ndege wawili kwa jiwe moja – yaani kupenda kusoma na pia kujifunza Kiingereza
bila shuruti. Au unasemaje Profesa Mbele?
Enzi hizo hamasa ya
kusoma vitabu vya riwaya vya Kiingereza ilikuwa kubwa mno kiasi hata kulikuwa
na mashindano ya nani kasoma “Chase” nyingi kuliko wenzie. Binafsi nimesoma “Chase”
kama 30 hivi, na steringi wangu niliyempenda
sana ni Mark Girland, nikianza na kitabu cha “This is for Real” na
baadaye “Have this one on me”, “You have yourself a deal”na “The Whiff of money”.
Vic Malloy pia nilipenda visa vyake.
Pamoja na kumsoma
sana James Hadley Chase, wengi wetu hatukujisumbua kumjua yeye ni nani, zaidi
ya kuburudika na riwaya zake za kusisimua, ambazo nina uhakika zilihamasisha
hata waandishi wetu kina Elvis Musiba , Ben Mtobwa, Hammie Rajabu, Eddie Ganzel ambao sasa wote ni
marehemu – ila vitabu vyao bado vingali hai.
Tukirudi kwa James
Hadley Chase mstuko wa kwanza utaokupata ni kwamba yeye jina lake halisi
halikuwa hilo ambalo alilitumia kiuandishi tu. Jina lake lilikuwa René Lodge
Brabazon Raymond. Alitumia pia majina mengine ya kiuandishi kama vile James
L. Docherty, Raymond Marshall, R. Raymond na Ambrose Grant.
Pamoja
na hayo Chase aliibuka kuwa mwandishi mashuhuri wa riwaya, akiwa ameandika
jumla ya vitabu 90, na kujulikana kama mfalme wa riwaya za kusisimua barani
Ulaya na duniani kote, ambapo riwaya ya vitabu vyake 50 zilichezewa filamu.
René Lodge Brabazon
Raymond (James Hadley Chase) alizaliwa Desemba 24, 1906 huko London, Uingereza., akiwa mtoto wa
mwanajeshi wa jeshi la kikoloni la India Kanali Francis Raymond. Huyu baba akiwa daktari wa
mifugo, alipania mwanae asomee sayansi pia, na kumpeleka shule ya King's School,
Rochester, huko Kent.
Hata hivyo Chase aliondoka nyumbani akiwa na umri wa miaka 18. Mwaka 1932 alimuoa Sylvia Ray, nao wakajaaliwa mtoto wa kiume. Mwaka 1956 wakahamia Ufaransa, ambapo mwaka 1969 wakaenda kuishi Uswisi, wakiishi maisha ya kipweke maeneo ya Corseaux-sur-Vevey, katika ziwa Geneva. Chase alifariki huko Februari 6, 1985
Hata hivyo Chase aliondoka nyumbani akiwa na umri wa miaka 18. Mwaka 1932 alimuoa Sylvia Ray, nao wakajaaliwa mtoto wa kiume. Mwaka 1956 wakahamia Ufaransa, ambapo mwaka 1969 wakaenda kuishi Uswisi, wakiishi maisha ya kipweke maeneo ya Corseaux-sur-Vevey, katika ziwa Geneva. Chase alifariki huko Februari 6, 1985
Wakati wa vita kuu
ya pili ya dunia, Chase alijiunga na jeshi la anga na kupanda vyeo hadi kufikia
Kiongozi wa Skwadi (Squardon leader). Huko pia alikuwa akihariri jarida la
Jeshi la Anga la Uingereza, na kuandika riwaya kadhaa kutoka humo baada ya vita
katika kitabu kilichoitwa Slipstream: A Royal
Air Force Anthology.
Baada ya Chase kuondoka nyumbani akiwa na umri wa miaka 18, akawa
anafanya kazi za kuuza vitabu, hasa vya watoto, katika duka moja la vitabu.
Kabla ya kuanza kuandika riwaya, aliwahi kuwa mpiga picha wa kulipwa, na hobby
zake kubwa zilikuwa muziki wa classic na opera,
Matatizo ya
kiuchumi huko Marekani kati ya miaka 1929 na 1939, iliyopelekea kuwepo na Usongo
mkuu (Great Depression) kuliibua makundi mengi ya kijambazi. Hayo na
kuchanganya na biashara ya vitabu ya Chase, akagundua kuna fursa ya kuwa
mwandishi wa riwaya za kijambazi.
Na baada ya kusoma kitabu cha James M. Cain
cha “The Postman Always Rings Twice cha mwaka 1934, na baada ya kusoma hadithi
ya kundi la kijambazi liloongozwa na mwanamke aitwaye Ma Barker na watoto wake,
akaandika kitabu chake cha kwanza cha riwaya za kusisimua kilichoitwa “No
Orchids for Miss Blandish. Kitabu kilipanda chati sana na kuweza kuwa bora kwa
mwongo mzima. Kuanzia hapo kitabu kimoja baada ya kingine kikafuata hadi
kufikia 60.
Dah! Hapa bwana Kipingo whoever ur kwa kweli umenipeleka Ikulu. Kwanza ni kweli sikuwahi kumuona huyu Chase kama alivyo. Pia naomba hata Profesa Mbele hajajibu nikwambie kwamba siku hizi watu wanadhani mtandao ndio mwisho wa matatizo ya kusoma. Zamani usipotoa stori za Chase kijiweni wewe ulikuwa unaonekana fala tu. Uzuri wa mada hii ni kwamba mtu mavitabu ya elimu (text books) pekee hupati stimulation ya kusoma hata mistari miwili. Sie shuleni kila Ijumaa ulitakiwa ulete review ya kitabu ulichosoma cha hadisi.Sijui kama ipo siku hizi. Ila the bottom line ni kwamba ili kurejesha utanmaduni wa kusoma vitabu lazima usome vitabu vya kusisimua kama Chase. Mitaani vipo kibao. JARIBU UONE!!
ReplyDeleteAsanteni kwa kunikumbuka. Namshukuru Sultani Kipingo kwa makala yake. Nami imenikumbusha mbali.
ReplyDeleteNilipokuwa nasoma Mkwawa High School, 1971-72, hali ilikuwa hivyo hivyo alivyoelezea Sultani Kipingo kuhusu kupendwa kwa riwaya za James Hadley Chase. Kwa kweli, sina la kuongeza.
Nakushuru pia ndugu "anonymous" kwa hayo uliyosema. Tuko pamoja.
Thanks to African Writers Series, David Maillu ( My dear Bottle) After four Thirty and many more, and Chase. I remember his writing he was so descriptive, he described streets so well, especially parts of the USA. Seriously technology has served us well, but it has also robbed us of imagination.
ReplyDelete