Katibu wa CCM Mkoa wa Singida Naomi Kapambala akizungumza na waanndishi wa habari juu ya ufafanuzi wa maendeleo ya ujenzi wa uwanja huo.
Na Hillary Shoo, Singida
Mbunge
wa Jimbo la Singida mjini (CCM), Mohammed Dewji ameulalamikia uongozi
wa Chama chake Mkoa wa Singida kwa kitendo cha kuchelewesha mchakato wa
kumalizia ujenzi wa Uwanja wa michezo Namfua ikiwa ni moja ya ahadi
zake alizotoa kwa wananchi wakati wa Uchaguzi Mkuu mwaka 2010.
Kuchelewa
huko kuanza kwa mchakato wa ukarabati na uwekaji wa nyasi za bandia
kwenye uwanja huo imeelezwa ni kutokana na urasimu na maslahi binafsi
miongozi mwa viongozi wa CCM Mkoa wa Singida.
Katika
barua yake ya Julai 31 mwaka huu kwa Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman
Kinana, Dewji amedai kuwa kwa kiasi kikubwa ameweza kutekeleza Ilani ya
Uchaguzi kwa vipindi vyote viwili pamoja na ahadi zake binafsi,
isipokuwa ahadi ya kumalizia ujenzi wa michezo Namfua.
Katika
barua hiyo, ambayo pia ameinakili kwa Rais Jakaya Kikwete, Katibu
Baraza la wadhamini CCM Taifa, Katibu wa Uchumi na Fedha na Katibu wa
CCM mkoa wa Singida, Dewji amedai kuwa kila alipotaka kufanya hivyo
alipata vikwazo kutoka kwa viongozi wa CCM mkoa wa Singida.
HABARI ZAIDI BOFYA HAPA
HABARI ZAIDI BOFYA HAPA
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...