Narudi katika safu hii kwa ngoma ya "Kuch Kuch Hota Hai"

Na Sultani Kipingo
Kuch Kuch Hota Hai  (tafsiri yake “kuna vitu hutokea”), ambayo pia ilijulikana kama KKHH, ni filamu ya kuchekesha ya Kihindi iliyotoka India na Uingereza Oktoba 16, 1998. Mwandishi na mwongozaji wake alikuwa Karan Johar na wachezaji wake walikuwa Shahrukh Khan na Kajol, ikiwa ni filamu yao ya nne pamoja. Ilipigwa India, Mauritius na Scotland, ikiwa ni mara ya kwanza kwa Karan Johar kuongoza filamu, akiwa na lengo la kupiga hatua mpya katika filamu za Kihindi.
Hadithi yake inahusisha pembe tatu za aina mbili za mapenzi. Nusu ya kwanza inahusu marafiki wakiwa chuoni, wakati nusu ingine inaelezea hadithi ya binti wa mjane anayejaribu kuwaunganisha baba yake na rafiki wa zamani.
Filamu hii ilifanikiwa sana India na ulimwenguni kote, ikawa ndiyo filamu iliyoingiza mapato makubwa kwa mwaka huo wa 1998, na pia filamu ya kwanza ya kihindi kuingia katika filamu 10 bora za Uingereza. Wakati muziki wake nao uliuza sana kwa mwaka huo, filamu hii ilijishindia tuzo kibao. Na hadi leo, pamoja kuwa ni ya siku nyingi, bado inatazamwa katika TV za India.



Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Tunaipataje hiyo? jamani enzi za majumba ya cenema zilikuwa juu pia .... umetukumbusha delight cinema ya shinyanga enzi zile tuko shycom

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...