Naibu Mtendaji Mkuu, Ofisi ya Rais-Usimamizi wa Utekelezaji wa Miradi (Presidents Delivery Bureau - PDB)
inayosimamia Mpango wa Matokeo Makubwa Sasa (Big Results Now! - BRN), Bw. Peniel Lyimo, akifungua
semina ya siku nne, ya tathmini ya Utekelezaji wa BRN kwa Mwaka wa kwanza; inayohusisha watendaji kutoka
wizara na sekta mbalimbali zinazotekeleza BRN. Semina hiyo imefunguliwa leo Jumatatu jijini Dar es Salaam.
Sehemu ya washiriki wakifuatilia mada katika semina hiyo ya tathmini inayohusisha watendaji wa BRN
iliyofunguliwa jijini Dar es Salaam leo Jumatatu. Semina hiyo inayowakutanisha watendaji wapya wa PDB na
BRN pia inahudhuriwa na maofisa wanahohusika na utekelezaji katika ngazi ya Wizara, Taasisi na Mikoa.
Watendaji kutoka Ofisi ya Rais-Usimamizi wa Utekelezaji wa Miradi (PDB) wakijadiliana jambo wakati wa
semina ya tathmini inayohusisha watendaji wa BRN iliyofunguliwa jijini Dar es Salaam leo Jumatatu. Kutoka
kushoto ni Meneja Mawasiliano na Utetezi, Bw. Hassan Abbasi, Mkurugenzi wa Huduma za Utawala wa PDB,
Bw. Maharage Chande na mtaalamu wa PDB kutoka PEMANDU Malaysia, Bw. Marc Shien Loong.
Naibu Mtendaji Mkuu wa PDB, Bw. Peniel Lyimo (kulia) akijadiliana jambo na baadhi ya watendaji wake wanaosimamia sekta ya kilimo katika BRN. Kutoka kushoto ni James Ngwira kutoka PDB, Bw. January Kayumbe Mkuu wa Kitengo cha Utekelezaji wa BRN katika Wizara ya Kilimo na Bw. Henry Kinyua, Mkurugenzi wa Idara ya Kilimo - PDB.
Naibu Mtendaji Mkuu wa PDB, Bw. Peniel Lyimo (kulia) akijadiliana jambo na baadhi ya watendaji wake wanaosimamia sekta ya kilimo katika BRN. Kutoka kushoto ni James Ngwira kutoka PDB, Bw. January Kayumbe Mkuu wa Kitengo cha Utekelezaji wa BRN katika Wizara ya Kilimo na Bw. Henry Kinyua, Mkurugenzi wa Idara ya Kilimo - PDB.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...