Na Greyson Mwase, Bagamoyo

Imeelezwa kuwa Tanzania inatarajia kuwa kitovu kikuu cha madini ya vito barani Afrika baada ya kubainika kuwa na utajiri mkubwa wa madini ya vito. Hayo yalisemwa na mtaalamu wa madini ya vito na almasi kutoka Kitengo cha Uthamini wa Madini ya Vito na Almasi (TANSORT) kilicho chini ya Wizara ya Nishati na Madini Teddy Goliama kwenye semina iliyoshirikisha Makamishna Wasaidizi wa Madini wa Kanda, Afisa Madini Wakazi na Wataalamu kutoka Wizara ya Nishati na Madini inayoendelea mjini Bagamoyo.

Goliama alisema Tanzania kupendekezwa kuwa kitovu kikuu cha madini ya tanzanite ni matunda ya ziara iliyofanywa na Kitengo cha TANSORT kwa kushirikisha wataalamu wa wizara ikiwa ni pamoja na ushiriki wake katika maonesho ya kimataifa ya vito ya Thailand yajulikanayo kama Bangkok Gem and Jewellery Fair.

Alisema sababu zilizopelekea Tanzania kupendekezwa kuwa kitovu cha biashara ya madini ya vito Afrika ni kutokana na wingi na aina mbalimbali za madini hayo pamoja na madini hayo kupendwa na wafanyabiashara wengi kutoka Thailand na nchi nyinginezo duniani.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...