KAMPUNI ya Tanzania Distilleries Ltd (TDL) imeendelea
kujitanua katika soko nchini baada ya kuzindua kinywaji kipya cha
kimataifa kiitwacho Fyfe's Scotch Whisky.
Akizungumza
katika hafla ya uzinduzi wa kinywaji hicho Dar es Salaam jana,
Mkurugenzi Mtendaji wa TDL, David Mgwassa alisema Fyfe's ni kinywaji
maridhawa kinachoandaliwa kikamilifu kikiwa na radha murua na ya kipee.
"Ubora
wa kinywaji hiki unatokana na umahiri mkubwa wa waandaaji na pia
unatokana kimea na nafaka bora zilizotumika na kuwa Fyfe's Whisky
huvundikwa kwa miaka kadhaa katika mji Loch Lomond, Scotland ili
kuongeza ubora wake kabla ya kuwa tayari kwa matumizi" alisema Mgwassa.
Mgwasa
aliongeza kuwa kampuni yao imekuwa ikiwaletea watanzania vinywaji
mbalimbali ambavyo vimekuwa chachu katika kusherehekea hatua tofauti za
mafanikio yao na kuendelea kuwaletea ladha tofauti za vinywaji bora.
Alisema
kinywaji hicho ni zawadi ya pekee katika soko na kuwa Tanzania imekuwa
nchi ya kwanza ulimwenguni kuzinduliwa na baadaye kitazinduliwa nje
nyingine.
Mkurugenzi Mtendaji wa TDL, David Mgwassa, akizungumza na wadau mbalimbali wakati wa hafla ya uzinduzi wa kinywaji hicho.
Langa Khanyile akitoa ufafanuzi wa Whisky hiyo kabla ya uzinduzi.
Sehemu ulipo fanyika uzinduzi huo katika Hoteli ya Serena.
Mkurugenzi
Mkuu wa Kampuni ya Tanzania Distilleries Ltd (TDL), David Mgwassa (wa
pli kushoto), akiwa na baadhi ya wageni waalikwa katika hafla ya
uzinduzi wa kinywaji kipya kiitwacho Fyfe’s Scotch whisky, iliyofanyika
Dar es Salaam juzi. Kushoto ni Mkuu wa Kitengo cha Masoko wa Kiwanda cha
Bia Tanzania (TBL), Kushila Thomas.
KWA PICHA ZAIDI BOFYA HAPA
KWA PICHA ZAIDI BOFYA HAPA
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...