Na Daud Manongi, WHVUM
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Mizengo Pinda anatarajiwa kuwa mgeni rasmi
katika uzinduzi wa mashindano ya Kimataifa ya mchezo wa Wushu (Kung fu) yatakayofanyika hapa nchi
kuanzia tarehe 30 hadi 31 katika viwanja vya Mnazi Mmoja.
Hayo yamebainishwa na Rais wa Chama cha Mchezo wa Wushu nchini Mwalami Mitete alipokuwa
akiongea na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam.
Katika taarifa yake Mwalami alisema kuwa mashindano hayo yatajumuisha vilabu vyote vya mchezo huo
hapa nchini ambapo alitaja idadi yake kuwa 23 na kuongeza kuwa kutakuwa na timu shiriki kutoka nchi
mbalimbali zikiwemo China, Kenya, Uganda, Zimbabwe, Ethiopia, Libya na Iran.
“Tunatarajia kufanya mashindano ya Kimataifa ambayo yatajulikana kama 2nd
Wushu Competition na yatafanyika kuanzia tarehe 30 na 31 kuanzia saa 4 asubuhi mpaka saa 12 jioni
katika viwanja vya Mnazi Mmoja”. Alisema Mwalami.
Kwa upande wake Mwakilishi wa Serikali kupitia Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Bw.
Michael Kagondela amesema kuwa ni fursa nzuri kwa wadau wa michezo hapa nchini hasa wa mchezo
wa Wushu kwa kuaandaa mashindano makubwa yanayoshirikisha timu kutoka sehemu mbalimbali
kwani kufanya hiyvo kutaongeza hamasa kwa wanamichezo wa Tanzania kujifunza kutoka kwao
Aidha Kagondela ameupongeza umoja wa wafanyabiashara wa China hapa nchini kwa hatua yao ya
kudhamini mashindano hayo na kuomba wadau wengine wajitokeze katika kusaidia kukuza michezo
hapa nchini.
Mshauri wa Masuala ya Utamaduni kutoka Ubalozi wa China hapa nchini Liu Pong mshindano hayo
kufadhiliwa na Jumuiya ya wafanyabiashara wa China hapa nchini ni matunda ya ushirikiano wa muda
mrefu baina ya Tanzania na China na kuongeza kuwa michezo ni njia ambayo itaendeleza uhusiano huo.
Hii ni mara ya pili kwa chama hicho kuandaa michuano mikubwa ya mchezo huo baada ya awali kuandaa
michuano ya taifa iliyohusisha klabu pekee za Tanzania iliyofanyika Ufukwe wa Coco mwaka 2011.
Tanzania International
Mshauri wa masuala ya Utamaduni kutoka Ubalozi wa China nchini Tanzania wa pili kutoka kulia Bw.Liu Pong akiongea na wanahabari hawapo pichani kuhusu mashindano ya kimataifa ya mchezo wa WUSHU yatakoayofanyika kwenye viwanja vya mnazi mmoja mwezi wa nane jijini Dar es Salaam mwaka huu.
Mwakilishi wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Bw. Michael Kagondela watatu kutoka kulia akiongea na wanahabari hawapo pichani kuhusu mashindano ya kimataifa ya mchezo wa WUSHU yatakoayofanyika kwenye viwanja vya mnazi mmoja mwezi wa nane jijini Dar es Salaam mwaka huu
Rais wa Chama cha WUSHU nchini wapili kutoka kushoto akiongea na wanahabari hawapo pichani kuhusu mashindano ya kimataifa ya mchezo wa WUSHU yatakoayofanyika kwenye viwanja vya mnazi mmoja mwezi wa nane jijini Dar es Salaam mwaka huu
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...