Uongozi na wachezaji wa Timu ya Soka ya African Coast ya Kijiji cha Upenja umemuomba radhi Mbunge wa Jimbo la Kitope Balozi Seif Ali Iddi kufuatia uamuzi wa Timu hiyo kuruhusu kufanyika kwa Mkutano wa Hadhara wa Chama cha Upinzani uliozaa kashfa na matusi dhidi ya mbunge huyo.

Wachezaji hao waliomba radhi hiyo Mbele ya Mbunge huyo hapo katika Ukumbi wa Tawi la CCM la Kijiji cha Upenja kilichomo ndani ya Jimbo la Kitope Wilaya ya Kaskazini “B “ mkutano uliohudhuriwa pia na Wazee na baadhi ya viongozi waasisi wa CCM wa Kijiji hicho.

Akiwasilisha salamu hizo za kuomba radhi Msemaji wa Timu hiyo ya Soka ya African Coast Juma Mshamba alisema wachezaji na Viongozi wa clabu hiyo walifikia uamuzi wa kukutana na Uongozi wa Wazee wa Tawi hilo kwa lengo la kuomba radhi baada ya tukio hilo la mvua za matusi dhidi ya Viongozi wao.

Juma Mshamba alisema pamoja na nia safi ya Viongozi na Wachezaji hao ya kuruhusu Mkutano huo, lakini pia zilitumika mbinu za hadhaa kwa Viongozi wa upinzani kuahidi kuwapatia fedha za kuendesha klabu yao pamoja na kuwatengenezea uwanja wao mambo ambayo hakuna hata moja hadi sasa lililotekelezwa na chama hicho cha upinzani.

Akizungumza na Wazee, Viongozi na wachezaji hao wa African Coast Mbunge wa Jimbo la Kitope Balozi Seif Ali Iddi alisema tayari ameshawasamehe tokea wakati wa mshindano ya Jimbo la Kitope ya Kombe la ZAWEDA ambapo timu hiyo iliidhinishwa kushiriki kwenye mashindano hayo.

Balozi Seif ambae pia ni Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar aliwaasa wanamichezo hao kujiepusha na vitendo vyote vinavyoashiriadalili za uvunjifu wa amani katika maeneo yao.

Naye Mke wa Mbunge huyo wa Kitope Mama Asha Suleiman Iddi aliwatanabahisha wanamichezo hao kuwa mbali na udanyanyifu wa baadhi ya watu wanaowatumia wanamichezo katika kushiriki kufanya maovu mitaani.
Mzee wa Timu ya African Coast Ali Soud akipokea mchango wa Mbunge wa Kitope Balozi Seif kwa ajili ya kulipa deni ya kambi ya timu hiyo pamoja na ada ya timu, kadi za wachezaji pamoja na Mrajisi wa michezo.
Mbunge wa Jimbo la Kitope Balozi Seif Ali Iddi akimkabidhi Kepteni ya Timu ya Soka ya African Coast ya Upenja Ali Hassan Mipira,seti ya Jezi pamoja na Fulana za mazoezi kwa ajili ya wachezaji wa timu hiyo iliyomo ndani ya Jimbo lake.

Msemaji wa Timu ya Soka ya African Coast ya Upenja Wilaya ya Kaskazini “ B” Juma Mshamba akiomba radhi kwa Mbunge wa Jimbo la Kitope Balozi Seif hayupo pichani kufuatia uamuzi wa timu hiyo kuruhu uwanja wao kutumika kwa mkutano wa hadhara wa chama cha upinzani ulioporomosha matusi dhidi ya mbunge huyo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...