Mkurugenzi wa Huduma za Uanachama wa Tanzania Private Sector Foundation (TPSF)Louis Accaro akiongea na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam(hawapo pichani) kuhusiana na warsha ya kuboresha na kupanua huduma za kifedha itakayofanyika kesho/leo Serena Hotel jijini Dar es Salaam, wanaoshuhudia kutoka kushoto ni Mshauri wa TPSF Dk.Donath Olomi, Mkuu wa Idara ya Mawasiliano na Uhusiano wa Vodacom Tanzania Rosalynn Mworia na Kulia ni Mtaalamu wa Biashara wa FSDT Peter Kingu,Warsha hiyo imedhaminiwa na Vodacom Tanzania.
Mtaalamu wa Biashara wa Financial sector Deepening Trust(FSDT)akisisitiza jambo kwa waandishi wa habari(hawapo pichani) kuhusiana na warsha ya kuboresha na kupanua huduma za kifedha itakayofanyika kesho/leo Serena Hotel Dar es Salaam.Katikati ni Mkurugenzi wa Huduma za Uanachama wa Tanzania Private Sector Foundation (TPSF)Louis Accaro na kushoto ni Mkuu wa Idara ya Mawasiliano na Uhusiano wa Vodacom Tanzania Rosalynn Mworia.Warsha hiyo inadhaminiwa na Vodacom Tanzania.
Mkurugenzi wa Huduma za Uanachama wa Tanzania Private Sector Foundation (TPSF)Louis Vodacom Tanzania Rosalynn Mworia, Mshauri wa TPSF Dk.Donath Olomi na Mtaalamu wa Biashara wa FSDT Peter Kingu(kulia) mara baada ya mkutano na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam(hawapo pichani) kuhusiana na warsha ya kuboresha na kupanua huduma za kifedha itakayofanyika kesho/leo Serena Hotel Dar es Salaam na kudhamiwa na Vodacom Tanzania.
Zaidi ya wafanyabiashara 100 wadogo na wa kati wanakutanishwa na watoa huduma sekta ya fedha kesho (Jumanne Agosti 19, 2014) jijini Dar es salaam katika semina maalum iliyoandaliwa na Taasisi ya sekta bianfsi Nchini (TPSF) iliyofadhiliwa na Vodacom na FSDT.
Mkutano huo unaofanyika chini ya ufadhili wa Kampuni ya Vodacom na Taasisi ya ukuzaji sekta ya fedha nchini (FSDT) unafanyika katika hoteli ya Serena chini ya Uenyekiti wa Mwenyekiti wa TPSF Dk. Reginald Mengi.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es salaam Mkurugenzi wa Huduma za Uanachama wa TPSF Luis Akaro amesema shabaha ya semina hiyo ni kujadili vikwazo vya upatikanaji wa huduma za kifedha kwa wafanyabiashara na kubadilishana uzoefu.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...