Wabunge wa EALA wakiwasili The Guardian Ltd
Wabunge wa EALA wakipokea maelezo kutoka kwa mfanyakazi wa EATV na Radio walipotembelea vyombo vya Habari vya IPP jana
 Spika wa Bunge la Afrika Mashariki Dkt Margaret Zziwa akizungumza baada ya kupokea maelezo kutoka kwa mfanyakazi wa EATV na Radio wakati wa Ziara ya wabunge hao IPP Media. Wa nne kushoto ni Katibu Mkuu Wizara ya Ushirikiano wa Afrika Mashariki Bi. Joyce Mapunjo.

Wizara ya Ushirikiano wa Afrika Mashariki inapenda kuwataarifu wananchi kuwa Bunge la Afrika Mashariki litafanyika kuanzia Agosti 27 hadi Septemba 4 katika ukumbi wa Karimjee Jijini Dar es Salaam.
Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete anatarajiwa kulihutubia Bunge hilo siku ya ufunguzi Agosti 27.
Vikao vya Bunge hilo vitakua vikifanyika kuanzia saa 8.30 mchana siku za Jumanne, Jumatano na Alhamis.
Pamoja na Mambo mengine Bunge hilo litajadili Muswada wa Elimu ya Mtangamano wa Jumuiya ya Afrika Mashariki wa 2014 na pamoja na mambo mengine litapokea na kujadili ripoti mbalimbali.
Wizara inawakaribisha wananchi kufuatilia kwa karibu vikao vya Bunge la Afrika Mashariki ili waweze kujua mambo mbalimbali yanayohusu mtangamano wa Afrika Mashariki.

Imetolewa na:

KATIBU MKUU

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...