Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete akihutubia Baraza Kuu la 69 la Umoja wa Mataifa siku ya Alhamisi ambapo pamoja na masuala mengine alitoa wito kwa Jumuiya ya Kimataifa wa kutoinyanyapa Afrika kwa sababu ya Ebola na kusisitiza kuwa Afrika ni Bara la lenye nchi 53 na kwamba si nchi zote zenye Ebola kauli iliyopigiwa makofi na wajumbe wa Baraza Kuu la 69 waliokuwa wakimsikiliza ikiwa ni ishara ya kuunga mkono kauli yake.
Na
Mwandishi Maalum,
New York
New York
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe.
Jakaya Mrisho Kikwete ameungana na viongozi wengine duniani katika
kuichagiza Jumuiya ya Kimataifa kuzisaidia Liberia, Siera Leone na Guinea mataifa ambayo yameathirika vibaya
na mlipuko wa Ugonjwa wa Ebola. Amesema misaada inayopelewa na itakayopelewa katika nchi hizo inatakiwa kuwa endelevu na ya uhakika hadi
pale ugonjwa huo utakapodhibitiwa.
Rais
Kikwete ametoa wito huo siku ya alhamisi wakati alipokuwa akilihutubia Baraza
Kuu la 69 la Umoja wa Mataifa katika majadiliano ya jumla ( General Debate) yaliyoanza siku ya jumatano hapa Makao Makuu ya Umoja wa
Mataifa. Akaongeza pia kwamba
nchi za Afrika ya Magharibi na nyingine barani Afrika zinatakiwa
kujengewa uwezo ukiwamo wa namna ya kuchunguza ugonjwa huo, kuwa na maeneo maalum ya wagonjwa pamoja na huduma za matibabu. Kwa
mujibu wa Rais Jakaya Kikwete juhudi
zaidi zinatakiwa kufanyika za kufanikisha
upatikanaji wa tiba ya uhakika ya ugonjwa huo, tiba ambayo amesema
itasaidia pia kuimarisha afya za wale ambao tayari wameathiria.
Akizungumzia
zaidi kuhusu mlipuko wa Ebola na athari zake,
Rais ametaka kuwapo kwa ushirikiano ndani ya
jumuiya ya kimataifa hususani
nchi zenye uwezo mkubwa wa kifedha na utaalam
ili kwa umoja wao waweza kuwasaidia
wanasayasi ambao wanaendelea na jitihada za kutafuta tiba na chanjo ya
ugonjwa wa Ebola. Pamoja
na kutaka mataifa
yaliyoathirika na Ebola kusaidiwa kwa hali na mali, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzani ameitaka pia Jumuiya ya
Kimataifa kutoinyanyapaa Afrika kwa sababu ya Ebola.
Akasema taarifa za kuwapo kwa watu wanaofuta au kuahirisha
safari zao za kwenda Afrika eti kwa sababu ya Ebola zinasikitisha.“Umoja
wa Mataifa na Marafiki wa Afrika,saidieni
kuwaeleza kwamba Afrika ni
Bara lenye nchi 53.Afrika siyo nchi moja, Nchi nyingi ziko mbali sana na nchi
nchi ambazo zimeathirika kwa Ebola. Na kwa kweli pengine nchi zilizoathirika ziko karibu zaidi na Ulaya kuliko mataifa mengine ya Afrika”.
Akaongeza “Tusaidieni kupaza sauti ya Afrika ya
kutonyanyapaliwa kwa sababu ya Ebola” akasema
Rais. Kauli iliyopigiwa makofi na wajumbe waliokuwa
wakimsikiliza.
Katika
hotuba yake pamoja na kuuzungumzia
kwa kina
mlipuko wa Ebola, Rais Kikwete
pia alizungumzia kuhusu maeneo mengine
muhimu hususani katika Usalama wa Kimataifa, ambapo aligusia matukio ya kigaidi
yanayoendeshwa na makundi kama Al
Shaabab, ISIS na Boko Haram katika maeneo mbalimbali na kwamba makundi hayo
hayapashwa kuachwa kuendelea na uovu wao.
Akayataja maeneo mengine ambayo yanaendelea kuifanya
dunia kutokuwa mahali salama kuwa ni
pamoja na mwendelezo wa uvunaji haramu wa mali asili, uwindaji
haramu, biashara haramu ya dawa za
kulevya na silaha. Aidha ametoa wito wa kutafutiwa ufumbuzi wa kudumu
wa migogoro inayoendelea huko Libya,
Jamhuri ya Afrika ya Kati na Sudani ya Kusini. Kuhusu
Palestina Rais amesema dunia haihitaji
kusubiri zaidi hasa kutoka na mikasa
ambayo imesababisha maisha ya watu
wasiokuwa na hatia wakiwamo watoto, wanawake na wanaume kupotea bila sababu.
Na
kwa sababu hiyo ametoa wito wa Umoja wa Mataifa, Marekani, Urusi na Mataifa ya
mengine ya Ulaya yafikie mahali
pa kuutafutia ufumbuzi wa kudumu mgogoro
kati ya Palestine na Israel jambo
alilosema kuwa linawezeka.
Kwa
upande wa Sahara ya Magharibi ambalo ni koloni pekee barani Afrika, Rais
Kikwete ameiutaka Umoja wa Mataifa na wadau wengine kulitafutia
ufumbuzi ili nalo lifike tamati.Rais
pia alizungumza tatizo la muda mrefu la vikwzo vya kiuchumi ambavyo imewekewa
Cuba, akazungumzia pia tatizo na
changamoto ya mabadiliko ya Tabia
nchi,na mchakato wa maandalizi ya
malengo mapya ya maendeleo endelevu ambayo alisema Tanzania iko tayari kushirikiana na mataifa mengine katika eneo hilo.
Ugonjwa huu ni janga unaopashwa kuhamasisha waafrika wote kuboresha vituo vyetu vya afya.
ReplyDeleteSIJAMSIKILIZA AKIZUNGUMZA; KATUMIA LUGHA YETU? MANAKE SIYE NI WASWAHILI. KILA MMOJA NA LUGHA YAKE; KUWA NA LUGHA SI DHAMBI
ReplyDeleteSawa kabisa mdao wa kwanza. Halafu rais anasema Afrika isinyanyapaliwe kwa sababu ya Ebola. Watu wanaogopa na huku majuu hawajui hata Afrika bora rais kaelezea ila bado wezetu wa majuu kuelewa si rahisi. Waliona wale wagonjwa wa Ebola walivyoletwa huku marekani walivyofunikwa kama nusu maili ni ngumu sana kuelewa. Na kuzingatia hatuna vituo vya afya vya kueleweka ni shida tupo
ReplyDeleteMagonjwa mengi yanaletwa na tabia za watu wa eneo husika. Ebola imeletwa na ulaji wa nyama pori hususan nyama ya nyani ambayo ni maarufu Africa magharibi na Africa ya kati. Ugonjwa wa SAR uliletwa na ulaji nyama ya paka China. Magonjwa mengine yako kwa wanyama tu, yakiingia kwa binadamu huwa ni maafa na kwa kuwa Ebola ni ugonjwa wa Africa, huchukua muda kwa Dunia ku-react kama tunavyoshuhudia.
ReplyDeleteMdau wa nne hapo juu fanya utafikti kikamilifu kwanza kabla ya kufikia hitimisho kuhusu chanzo cha magonjwa hayo!!
ReplyDeleteJambo moja ambalo hatujaliweka vizuri hapa Afrika ni utegemezi wetu uliokithiri kiasi kwamba tunaweza kutoweka wote kama likitokea tatizo kubwa. Hatuwekezi kwenye maarifa na tafiti ya kutufanya tuwe self-reliant! Tatizo kidogo tu tunaomba jumuia ya kimataifa! Na huu ni uzembe wetu sisi wenyewe kwa kukosa visheni ya Bara letu. Hatuweki nguvu zetu pamoja kwenye kupanga! Utamsikiliza kila kiongozi wa Afrika akisimama anaongea mambo tofauti na mwingine, wakati sisi watawaliwa katika Afrika tuna mambo yanayofanana katika kujikwamua kwenye hizi changamoto tulizonazo! Sasa AU inakazi gani kama sio kwenda kujenga hoja ya pamoja? Enzi za Mwalimu, nchi za Afrika zilikuwa zinaenda UNO na ajenda moja, au zinazoshabihiana! Lakini kwa bahati mbaya sasa hivi inaonekana kana kwamba hawa watishi wametugawa kiasi kikubwa hadi baadhi ya viongozi wanapenda kutowaudhi wakubwa, hivyo wanaongea lugha laini.
We have common challenges but different voices! Nakumbuka Enzi za Thomas Sankara!!
Mataifa makubwa yataendelea kututawala hata kama tumepata uhuru,Uhuru wa nchi za kiaafrika Utabaki kuwa wa nadharia kwani hakuna dalili ya kujiondoa katika utegemezi na uegemezi wa mataifa haya. Na hakika hatutakuwa na wakumlaumu isipokuwa sisi wenyewe kwa kushindwa kusimamamia rasilimali zetu vyema kwa manufaa yetu wote.viongozi wa Africa wanakula mpaka wanasahau kutenga budget ya maafa. Kila kukicha kunapiga foleni na bakuli mkononi tukiomba misaada wakati tunarasilimali lukuki. Hata tukichekwa,au kusimangwa ni haki yetu.
ReplyDelete