Kampuni ya ufuaji umeme ya Independent Power Tanzania Limited (IPTL) na
wadai wengine wawili wamefungua kesi ya madai katika Mahakama Kuu dhidi ya
Mbunge wa Jimbo la Kigoma Kaskazini, Bw. Zitto Kabwe na wengine wawili wakitaka
kulipwa fidia ya Shilingi bilioni 500 kwa kashfa alizotoa kimaandishi dhidi yao.
Mbali na IPTL, wengine waliofungua kesi hiyo mnamo
tarehe 4, Septemba kupitia wakili Melchisedeck Lutema wa Asyla Attorneys na Kay Felician Mwesiga wa Bulwark Associates
Advocates, ni kampuni ya Pan Africa Power Solutions Tanzania Limited (PAP) na
Mwenyekiti Mtendaji wa makampuni hayo mawili, Bw. Harbinder Sing Seth.
Wadai
hao watatu, miongoni mwa mambo mengine wanahitaji malipo ya fedha kutoka kwa
Bw. Kabwe na washtakiwa wengine watatu ambao ni mhariri wa gazeti la Raia Mwema,
Kampuni ya Raia Mwema na kampuni ya Flint Graphics, kuwa kama fidia itokanayo
na makala ya kuwachafua iliyochapishwa kwenye gazeti hilo, iliyosababishwa na
washitakiwa hao.
Pamoja
na hayo, pia wanahitaji tamko rasmi toka mahakamani kwamba makala iliyokuwa na
kichwa cha habari "Fedha za IPTL ni Mali Ya Umma"
iliyochapishwa katika kurasa wa 7 na 14 za gazeti la tarehe 13 Agosti, 2014
ilikuwa ni ya kupotosha na kuchafua kwa kudhamiria na kuhitaji washitakiwa
kuomba radhi kwa kuandika na kuchapisha katika kurasa za mbele kichwa cha
habari ya kuomba msamaha katika matoleo mawili mfululizo ya gazeti hilo.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...