Kwa namna ya pekee tunakukumbuka mtoto wetu FLORA FLOWIN MKANULA kwa kuitwa na Mwenyezi Mungu tarehe 10 Septemba, 2013.

Ni mwaka mmoja sasa tangu ututoke. Upendo wako, ucheshi wako, ushauri wako, uvumilivu wako utakumbukwa daima na sisi wazazi wako Baba FLOWIN na Mama ALICE.

Unakumbukwa pia na wadogo zako, IRENE na CARRINE, Marafiki, Wanafunzi wenzio wa ‘PCB’ pamoja na familia ya ST. JOSEPH CATHEDRAL HIGH SCHOOL. Kwa hiyo siku ya Jumatano tarehe 10 Septemba, 2014 itaazimishwa Misa Takatifu Kinondoni Makaburini tukiwa na familia ya ST. JOSEPH CATHEDRAL HIGH SCHOOL saa 3.00 asubuhi, na baadae tutaenzi siku yake kwa maadhimisho yatakayofanyika mchana saa 7.30 ST. JOSEPH CATHERDRAL HIGH SCHOOL kwa nia ya kumshukuru Mungu kwa zawadi ya FLORA FLOWIN MKANULA.

“Bwana ametoa na Bwana ametwaa jina lake lipewe sifa”.

“AMINA”

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...